Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia hoja hii ya uwekezaji wa mitaji ya umma (PIC) kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, upungufu wa mitaji; Mashirika mengi na Taasisi za Umma hazina mitaji ya kutosha. Mfano Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB). Benki hii ingekuwa na mtaji wa kutosha ingepelekwa katika Mikoa yote ya Tanzania na ingeweza kuwainua Watanzania walio wengi, maana wakulima wengine kuliko wafanyakazi na wafanyabiashara, lakini Serikali haijachukua jitihada ya kutosha kuisaidia benki hiyo kwa kuipa mtaji wa kuweza kuendesha benki hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, benki ilianza na mtaji wa shilingi bilioni 60 ingawa mtaji ulioidhinishwa ni shilingi bilioni 800. Kiasi hicho ni pungufu kwa asilimia 92.5. Serikali inaishia kuahidi lakini haitekelezi. Naiomba Serikali kutimiza ahadi yake ya kupeleka pesa yote ambayo iliidhinishwa kwa ajili ya uendeshaji wa Benki ya Kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Serikali kutolipa madeni yake kwa wakati; Mashirika mengi yanashindwa kujiendesha na kukamilisha miradi yake kwa ufanisi kutokana na Serikali kukopa lakini inachelewa kulipa madeni hayo. Naishauri Serikali kulipa madeni yake kila inapokopa. Hii inasikitisha kuona Serikali ndiyo inayodidimiza uchumi wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikikopa fedha zake kwenye Mifuko ya Hifadhi za Jamii. Matokeo yake imedhoofisha mifuko hiyo, mfano PSPF. Naiomba Serikali ijirekebishe namna nyingine Serikali itadidimiza uchumi wa nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.