Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa ufupi sana nataka nizungumzie juu ya korosho zetu, hakika ni zao bora mojawapo la kimkakati, ambalo Serikali imewekeza na linafanya vizuri sana katika kumkomboa mkulima pamoja na Taifa kwa ujumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini hivi karibuni kulikuwa na allegations za mawe kuwepo katika magunia ya korosho kule Vietnam. Sisi kama Serikali hatujakaa kimya tumejipanga na kama Serikali pia tumeunda timu na tumewapa wiki mbili na tutapata majibu na wote watakaobainika tutawachukulia hatua kali na za kisheria na tuweze kujua adui yetu ni wa ndani ama ni wa nje. Kwa sababu hili ni suala la uhujumu uchumi, naomba niwaeleze Waheshimiwa Wabunge kwamba kama Serikali tunahakikisha kabisa kwamba zao la korosho ambalo ni zao mojawapo bora tunafika kiwango cha juu na tutakuwa katika ramani ya dunia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni suala zima la Mpango Mkakati wa Maendeleo ya Kilimo. Naomba niwaeleze Waheshimiwa Wabunge kwamba sisi kama Serikali tumejipanga kuhakikisha kwamba tunaandaa Mpango Mkakati wa Maendeleo ya Kilimo (ASDP II) na Waheshimiwa wote tutawaalika kwenye uzinduzi wa Mpango Mkakati huo wa Kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.