Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kupata fursa hii ya kuchangia hoja ambazo zimewekwa mezani. Kwanza kabisa nami nianze kwa kutoa pole kwa familia ya Marehemu Mzee wetu, Mzee Kingunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nitoe hongera sana kwa Wenyeviti wote watatu kwa kuwasilisha vizuri kabisa hoja za Kamati zao mbele ya Bunge lako Tukufu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie katika suala hili na moja kubwa ambalo nataka kuanza nalo ni hiki ambacho kinaelezwa kama mkanganyiko wakati hakuna mkanganyiko wowote ambacho ni kuhusu Kodi ya Majengo. Naomba niiseme vizuri na ikiwezekana nitumie dakika zangu zote saba na Waheshimiwa Wabunge naomba mnisikilize kwa umakini na kwa pamoja tunapofanya maamuzi tufanye

maamuzi tukiwa tunaelewa nini tunafanya ndani ya Taifa letu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, imesemwa vizuri mwaka 2016/2017, Serikali ilikuja hapa Bungeni na Sheria ya Fedha ya mwaka huo na tukaleta ndani ya sheria kodi hii ikusanywe na Mamlaka ya Mapato Tanzania lengo likiwa ni ufanisi. Tulipoleta tulifungua na akaunti maalum kwa ajili ya kuweka pesa hizi za Kodi ya Majengo katika Benki Kuu ya Tanzania. Tulifungua akaunti hiyo tukiwa na dhamira ya dhati ya kukusanya na kuzirejesha kule zilivyo na ndicho tulichokifanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kutokana na historia ambayo sio njema, imesemwa hata jana wakati Kamati ya LAAC na PAC walipowasilisha taarifa zao humu ndani kuhusu matumizi yasiyo mazuri kwenye Halmashauri zetu. Pesa za miradi zinazopelekwa hutumika ndivyo sivyo. Kama Serikali na Wizara ambayo tumepewa mamlaka ya kusimamia mambo ya fedha hatuwezi kuacha haya yanaendelea kutendeka ndani ya Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kKwa umakini mkubwa wa Serikali yetu ya Awamu ya Tano chini ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli anayechukia ufisadi, anayechukia ubadhirifu wa fedha za umma, ikaja ndani ya Bunge lako Tukufu na tukaleta hoja kwamba pesa hizi zikusanywe na Mamlaka ya Mapato na zitarejeshwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niisome sheria tuliyoipitisha, baada ya kukusanywa kwa ufanisi tukasema, the apportionment and disbursement of the proceeds collected under this section shall be made to a Local Government Authority based on its budget. Nini tunabishana ndani ya Bunge lako Tukufu, sheria iko wazi na ndicho tunachokifanya kama Wizara, ndicho tunachokifanya kama Serikali. (Makofi)


Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala hili, kwanza naomba nitoe caution kwa Bunge lako Tukufu, tumwogope kama ukoma mtu anayetaka kuligawa Taifa hili vipande vipande. Tumekusanya tumeonesha ufanisi, matumizi sio mazuri na nini tumefanya baada ya kukusanya, tunazirejesha kulingana na sheria ilivyotuelekeza, according to the budget of the Local Government Authority, ndicho sheria inavyosema. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, waambie tu watulie, tuwafundishe ili waweze kufahamu, hiki haiwezekani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa leo tukisema kule Geita wakusanye kodi kutoka kwenye madini ibaki Geita na kule Manyara Mererani wakusanye kodi inayotokana na Tanzanite ibaki Mererani hatutokuwa na Taifa na Dar es Salaam wachukue kodi yote inayotoka bandarini wapi Taifa hili linakwenda? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe mfano mmoja ambao umesemwa hapa bajeti ya maendeleo kwa fedha za ndani kwa Mkoa wa Dar es Salaam ni shilingi bilioni 14.2, nini Serikali tumefanya kwa pesa za ndani kwa Mkoa wa Dar es Salaam? Tumepeleka shilingi bilioni 11 ambayo ni asilimia 79, tunapeleka kwa Mkoa wa Dar es Salaam. (Makofi)


Mheshimiwa Mwenyekiti, tumepeleka shilingi bilioni 11, nini tumekusanya kwenye Kodi ya Majengo Mkoa wa Dar es Salaam. Kwenye Kodi ya Majengo Mkoa wa Dar es Salaam tumekusanya shilingi bilioni 10 na sisi tushapeleka shilingi bilioni 11, hii ndiyo Kodi ya Majengo tunayoulizwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wapi tunataka kuelekea? Jambo la msingi kabisa tunalotaka kulielewa hapa, tuwaulize hao wa Kinondoni wanaosema wao wakikusanya ni mradi upi Halmashauri ya Kinondoni iliwahi kutelekeza kupitia Kodi ya Majengo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, watutajie tu mradi mmoja na kwenye bajeti ya mwaka huu, ndiyo maana nasema watulie, watueleze bajeti item iliyosema tutakusanya Kodi ya Majengo kiasi hiki na itakwenda kujenga kitu fulani twende kwenye bajeti ya Halmashauri ya Kinondoni. Kwa hiyo, tusiwadanganye Watanzania, tukalikatakata Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe mfano mwingine mdogo kwenye kodi hii ili Waheshimiwa Wabunge tuelewane na tufanye maamuzi sahihi. Nini kimekusanywa Halmashauri ya Kinondoni kwa mwaka elfu mbili, Mheshimiwa Halima analidanganya Bunge lako, Halmashauri ya Kinondoni mwaka 2014/2015 ilikusanya shilingi bilioni tano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukapeleka kwenye maendeleo zaidi ya shilingi bilioni tisa, Kinondoni peke yake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaombe Wabunge wanaopenda haki, wanaotaka Taifa letu liendelee kuwa Taifa moja kama tulivyoapa, tushikamane kwa pamoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.