Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Albert Ntabaliba Obama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. ALBERT O. NTABALIBA – MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UWEKEZAJI NA MITAJI YA UMMA:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tunamshukuru Mwenyezi Mungu kutuwezesha kufika muda huu lakini kipekee nikushukuru wewe kwa kunipa nafasi asubuhi hii kuweza kuwasilisha taarifa ya Kamati. Kipekee niwashukuru Wabunge wote kwanza kwa kusikiliza taarifa yenyewe na pili kwa kuweza kuisoma na kuijadili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi niende kuwashukuru waliochangia taarifa hii. Taarifa hii imechangiwa na watu wengi, nitaenda mmoja baada ya mwingine. Naomba nianze kipekee kuwashukuru Serikali kwa response yao ya hotuba yetu na michango ya Waheshimiwa Wabunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bila kupoteza muda, naomba nianze na hoja za Serikali na nianze na hoja aliyowasilisha Waziri wa Fedha kwenye majibu yake, pale Kamati tulipoomba kwamba Gavana asiwe Mwenyekiti wa Bodi na tukawa tumependekeza kwamba kwa sababu ya good governance zitenganishwe hizi pillar mbili lakini kwa majibu ya Mheshimiwa Waziri wa Fedha ameonesha kwamba ni vizuri iendelee kuwa hivyo kama ilivyo na ame-cite kwamba 90% ya survey waliyoifanya Gavana ndiyo Mwenyekiti wa Bodi.

Kwa mtazamo wa Kamati tuliona kwamba huenda vingetenganishwa vingeweza kuleta ufanisi lakini naomba nikubaliane na majibu ya Serikali kwamba kama wataendelea kuifikiria na kuiona hivyo bado inaleta ufanisi, basi tunaiomba tuiache hivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini naomba kabisa nimpongeze Profesa Luoga, tulipoita Benki Kuu kuja kwenye Kamati yetu hakuweza kufika lakini kwa kweli alionesha concern kwa nini hakufika na akawa amesikitika kwa nini hakufika, aliwatuma Magavana wake. Tunaomba tumpongeze kwa sababau alionesha concern kubwa ya kuheshimu Bunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine la pili ambalo Mheshimiwa Waziri amesema ni huduma za mashirika kwamba mashirika mengine ni kwa ajili ya ruzuku. Kama Kamati tunakubaliana na majibu ya Serikali issue yetu ni kwamba kama mmesema kwamba mtaipa ruzuku na yanasaidia, kwa nini hampeleki fedha? Ndiyo hoja yetu. Tunajua mashirika 175 kati ya 269 yanapewa ruzuku lakini kwa nini Mheshimiwa Waziri fedha za kuendesha mashirika haya haziendi kwa wakati? Hiyo ndiyo hoja yetu, kwa hiyo, tunaomba mwendelee kuifanyia kazi ili muweze kui-solve hii changamoto ya Kamati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchangiaji mwingine alikuwa ni Mheshimiwa Sixtus Mapunda aliyejaribu kuelezea vigezo na kwa nini ATCL. Sisi tumesema kwenye ripoti yetu ATCL ni kampuni ambayo ina umuhimu mkubwa lakini katika miaka mitatu imeendelea kupata hasara. Hata kama itakuwa na faida nyingine kwa sekta nyingine lakini kama shirika na sisi kama Kamati ya Uwekezaji ni lazima tui-task management na bodi ihakikishe kwamba inaleta faida ina- turn out hizi loss ambazo zipo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunakubaliana na mawazo ya mchangiaji kwamba inazo faida nyingine kwa sekta nyingine, hizo hatukatai tunajua kwamba intention ya Rais ya kununua ndege na ataendelea kununua ndege na sisi tunaunga mkono katika ku-boost utalii lakini tunapokuja kwenye shirika lenyewe lile nalo tunalitaka liweze kuwa na faida. Tunapoangalia mizania yake tunataka na lenyewe shirika liwe na faida pamoja na kwamba lina other profits kwenye sekta nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili ameongelea mitaji, nipongeze nia nzuri ya Serikali, 2016 Serikali hii ilikuwa imewekeza trilioni 23 ambapo mwaka jana tulipata faida ya bilioni 422.9 lakini kwa 2017 mtaji umeweza kuongezeka mpaka kuwa trilioni 47.8 ambapo tumeweza ku-realize gawio la bilioni 845. Kwa hiyo, hii ni achievement kubwa, lakini tunaposema generally faida bado ni 1.9% ambayo ni ndogo. Kwa hiyo, bado ni wito wetu kuhakikisha kwamba wanaoendesha mashirika wana-task ya kuhakikisha faida ya mashirika hayo inaonekana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwingine aliyechangia ni Mheshimiwa Mary Deo Muro, yeye alikuwa anaongelea Bodi ya mashirika hasa aliongelea RAHCO na Elimu Kibaha. Kwenye ripoti yetu tumesema vizuri na ukiangalia kwenye bodi bado tunai-task Serikali, mfano, MSD ina miaka karibu miwili haina Bodi na sasa hivi nia njema ya Mheshimiwa Magufuli, Rais wetu ya kupeleka fedha ya kununulia dawa, nia njema aliyonayo Waziri wa Afya na Serikali nzima inapeleka fedha nyingi lakini hamna bodi iliyopo pale. Ni wajibu wetu kuwakumbusha kwamba bodi ya MSD iweze kuteuliwa. Wanashindwa kufanya investment kwa sababu decision zingine za investment zinahitaji endorsement ya bodi. Sasa bodi hamna tunashangaa kwa nini uteuzi haufanyiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile Mheshimiwa Lolesia Bukwimba na Mheshimiwa Juma Hija wameongelea mambo ya madeni makubwa ambayo Serikali inadaiwa. Kwa hiyo, tunawakumbusha, kwenye ripoti yetu tuko so clear kwamba Serikali iweze kuanza kuchukua hatua za kuyalipa madeni hayo kwa mpangilio ambao inaona inaweza kuanza kuyalipa. Madeni yamekuwa makubwa, yanafanya makampuni, mashirika na taasisi zetu zishindwe kujiendesha na ku-meet target zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, yako mashirika ya umma ya Serikali ambayo ni wakandarasi lakini Sheria ya Manunuzi iliyopo inawaona kama ni mashirika au taasisi wanaonunua lakini kumbe ni wakandarasi. Tunayo TBA, DDCA, JKT, haya yote ni makampuni makandarasi, lakini kulingana na Sheria ya Manunuzi wanaonekana kama ni wanunuzi. Kwa hiyo, tunaomba kupitia Ofisi ya TR iweze kuandaa mapendekezo mazuri ambayo yataendana na mashirika haya kwani yanakosa biashara nyingi kwa sababu sheria inawabana na shughuli zinakuwa za muda mfupi. Kwa hiyo, Kamati bado inasisitiza hilo liweze kufanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, yako mashirika au kampuni ambazo hazijamtambua Msajili wa Hazina. Hapa ni msisitizo kwamba kupitia Ofisi ya TR basi aweze kuzikumbusha kwa sababu sheria zilizoanzisha mashirika haya nyingine ni za muda mrefu na TR ameanza kupewa uwezo muda siyo mrefu. Kwa hiyo, tungependa zile sheria ziweze kuwa reviewed iweze kuwekwa addendum ya sheria nyingine ili iweze kuzitambua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni wito wetu kwa Wizara ya Fedha kwani haitendi haki kwenye Ofisi ya Msajili wa Hazina. Kwanza hawana manpower, hawana watu wengi wenye weledi wa kuweza kuchambua mambo yote yaliyopo kwenye uwekezaji wa mitaji ya umma. Tuisihi Wizara ya Fedha iweze ku-empower Ofisi hii na iweze kuipa bajeti ya kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, Ofisi ya TR ilitakiwa iwe imetupa ripoti ya mwaka na hiyo ripoti ingeweza kuletwa kwa Waziri wa Fedha ambaye angeileta Bungeni na baadaye Kamati kupewa, lakini sasa ni miaka miwili na nusu hatujapokea ripoti hii. Sasa tunaiomba Wizara ya Fedha iweze kuijali na kuipa kipaumbele Ofisi ya TR.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mengine makubwa yaliyoongelewa ni madeni, mambo ya ndege, Bodi za Wakurugenzi tumeiongelea, iko kwenye ripoti yetu, Sheria ya Manunuzi tumeisema iko so clear na iko kwenye ripoti yetu. Kwa hiyo, nawashukuru hawa walioboresha ripoti yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Rhoda Kunchela amezungumzia Serikali kutolipa madeni kwa wakati, ni kweli, yako mashirika madeni ya DAWASCO, DUWASA na umeme. Kwa hiyo, haya ni mambo ambayo yanaweza yakazungumzwa ndani ya Serikali na tukaondokana na hizi embarrassment. Wananchi wanakatiwa huduma za maji kwenye visima, wanakuta kuna mgogoro Serikali haijalipa umeme, ni mambo ambayo mnaweza mkayaongelea ndani ya Serikali ili wananchi wasiweze kuathirika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Janet Mbene ameongelea mashirika yaendeshwe kibiashara, ni kweli na sisi tunasisitiza hilo na ndiyo maana ya kuanzisha Kamati hii ili iweze kuangalia mujarabu wa biashara kwenye mashirika haya. Kuhusu vigezo vya appointment, kuona mtu mwenye uwezo wa kuongoza shirika, nafikiri hilo nalo liendelee kuzingatiwa kama ulivyolitolea ufafanuzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, yako mengine ni ya jumla ambayo kwa kweli tunashukuru kwamba yameweza kuboreshwa, mengine wote walikuwa wanarudia karibu maeneo yaleyale. Kitu muhimu tunachosisitiza kama Mitaji ya Umma tunaomba mapendekezo tuliyoyatoa kwenye ripoti yetu Bunge iyaazimie, iyachukue na yawe ya Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naomba sasa niliombe Bunge lako Tukufu liweze kukubali mapendekezo yetu na hoja zetu ambazo zimetolewa ndani ya ripoti yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bila kupoteza muda, naomba kutoa hoja.