Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017.

Hon. George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017.

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Naibu Spika nakushukuru sana kwa kunipa nafasi, na nimshukuru sana Mheshimiwa Mbunge kwa kunipa hizi dakika tano. (Makofi)

Kwanza kabisa nizungumzie REA. REA awamu ya kwanza, REA awamu ya pili usimamizi wake haukua mzuri ndiyo maana miradi mingi ilikwama. Kwa mfano kuna vijiji vya Tambi, Nambori, kijiji cha Saa Zima, kijiji cha Igoji Moja na Igoji Mbili, tayari nguzo zipo na nyaya zipo lakini transformer hakuna. Kwa hiyo nilikuwa naomba sana katika REA hii ya awamu ya tatu waweke transformer ili wananchi waweze kupata huduma.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine, kuna vijiji ambavyo havijafikiriwa kabisa kupata umeme. Kijiji cha Kiboriani, Ngaramilo, Mkanana, Chamanda pamoja na Iwondo hazijapelekwa nguzo wala nyaya. Kwa hiyo naomba sana hii REA awamu ya tatu wawakumbuke basi wapate umeme.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la tatu, kukatika katika kwa umeme Mji wa Mpwapwa na maeneo mengine imekuwa ni kero kubwa sana, kila wakati kwa siku umeme unaweza kukatika mara mbili/tatu. Sasa kwanza unaweza kupata hasara ukaunguza vitu kwenye fridge, lakini pili kwa sababu wananchi wanalipa bill kwa hiyo lazima huduma ya umeme iwe nzuri. Sasa kisingizio cha TANESCO kwamba kwa sababu ya mvua na kuna baadhi ya nguzo zipo kwenye mabwawa, nguzo zingine zimeoza.

Mimi nashauri wabadilishe nguzo zote zile ambazo zimeoza. Kama inawezekana nguzo ziwekwe za chuma ambazo haziwezi kuoza, haziwezi kuliwa na mchwa hii inaweza kusaidia sana ili wananchi waweze kupata huduma ya umeme Wilaya ya Mpwapwa na Mkoa wa Dodoma kwa ujumla. Kwa hiyo ya kwangu yalikuwa ni hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi, ahsante sana.