Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017.

Hon. Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017.

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi kuchangia. Kwanza nawashukuru Wenyeviti wa Kamati, Mawaziri wote wa Wizara hizi tatu na Watendaji wao na Manaibu Waziri kwa kazi nzuri ambayo wanatufanyia.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuchangia nijielekeze kwenye Wizara ya Nishati. Wizara ya Nishati kuna maeneo mawili; kuna eneo la Densification na eneo la REA III, lakini yote inatoka kwenye REA. Kasi ya utendaji kazi wa Wakandarasi katika Jimbo la Bunda kwa upande wa densification ni mdogo sana, ninavyozungumza hapa, wako site lakini wanaenda pole pole sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, REA katika vijiji, kasi yake nayo imekuwa ndogo ingawa Mheshimiwa Waziri anafanya kazi kubwa sana ya kuanzisha hii miradi katika maeneo mbalimbali. Nami wakati fulani namhurumia, anatembea sana, lakini Wakandarasi wanaenda slow sana. Sasa, sijui ni upungufu wa hela au ni nini, sielewi.

Mheshimiwa Naibu Spika, namwomba Mheshimiwa Waziri sasa awahimize hawa Wakandarasi katika maeneo na hasa Wilaya ya Bunda, hususan Jimbo la Bunda katika maeneo ambayo Mheshimiwa Waziri alikuja akafanya uzinduzi wa Mradi wa REA III katika eneo la Maiwanda katika Jimbo la Bunda. Kwa hiyo, nafikiri ni vizuri Mheshimiwa Waziri akahimiza wakaja kwenye kutenda hiyo kazi vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika REA kuna mambo huwa siyaelewi vizuri. Moja, ni kitu kinaitwa kilometa. Unakuta kuna upungufu kati ya watu wa survey ya TANESCO na survey ya Mkandarasi, TANESCO ukiwauliza, nani amefanya survey ya kumpa Mkandarasi aende kujua Kijiji ‘A’ kila kilometa tatu, kina kilometa moja na Kijiji ‘B’ kinawekewa transfoma mbili na Kijiji ‘A’ kinapewa transfoma tatu au kilometa mbili. Sasa ukiuliza TANESCO, wanasema ni REA; ukiuliza REA, wanakuja na takwimu, hawahusishi wanakijiji wale kujua toka mwanzo kwamba kijiji hiki kitapata kilometa mbili au mtandao wa umeme wa kilometa mbili na transfoma tatu na voti ngapi katika hiyo transfoma. Kwa hiyo, hilo nalo ni tatizo liko hapa, Mheshimiwa Waziri naomba uliangalie vizuri ili tuweze kwenda vizuri katika suala hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna suala la Wizara ya Miundombinu. Kuna masuala ya barabara ya lami kutoka Nyamswa kwenda Bunda na kutoka Bunda kwenda Bramba na Bramba kwenda Kisorya, imechukua muda mrefu sana. Kwa hiyo, tunaomba Mheshimiwa Waziri anayehusika aweze kuiangalia kwa makini zaidi kwenye hiyo barabara. Kuna barabara ambayo inatoka Sanzati kwenda Mgeta na Mgeta kwenda Nata, nayo tunaomba Mheshimiwa Waziri anayehusika aweze kuiangalia vizuri hiyo barabara.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kusema mambo yafuatayo:-

Kwanza, ni kumpongeza Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri anayoifanya kwenye Mkoa wa Mara. Sisi Mara hatuna upungufu wa kupata Rais, tumewahi kupata Rais miaka 24, kwa hiyo, hatuwezi kulalamika kwamba Rais amefanya nini kwa miaka miwili iliyokuwepo hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimewahi kwenda India kumshuhudia mtu anafanyiwa operesheni; kuna operesheni ndogo na kubwa. Operesheni kubwa ni zile zinazohusisha matumbo kwa ndani; unatoa labda figo na vitu vingine. Mtu yeyote atakayekatwa kisu kwa operesheni kubwa lazima agune na lazima arushe miguu. Kwa hiyo, ninachoona wenzangu hapa wanarusharusha miguu, naona kama operesheni ya Mheshimwia Dkt. Magufuli imewafikia. Kwa hiyo, sioni matatizo ya namna hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Mheshimiwa Rais kwa mambo yote anayoyafanya. Kwanza, ni kutupa Mkoa wa Mara shilingi bilioni 10 za uwanja wa ndege. Kwa mara ya kwanza Rais, Mheshimiwa Dkt. Magufuli akiwa madarakani, juzi Waziri Mkuu ametua pale na ndege kubwa. Sasa tunamlaumuje kwa mambo haya? Tunapozungumza, site watu wanaendelea na kazi. Tunamshukuru Mheshimiwa Rais kwa kutuletea Mkoa wa Mara shilingi bilioni nne kwa ajili ya Hospitali ya Kongwa ambayo imekuwepo toka mwaka 1975. Inaendelea kufanya kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Niabu Spika, kwa hiyo, sisi Mara tunamlaumu kwenye jambo gani? Kwa hiyo, mambo mengine yapo, yanaendelea. Naona watu wanarusha miguu tu, lakini hali ya hewa ni nzuri. Kwa hiyo, namshukuru Mheshimiwa Rais pia kwa kudhibiti rushwa, kuweka nidhamu ya kazini, kudhibiti wazembe na wala rushwa, kutoa elimu bure, kuanzisha miradi mikubwa ya Stigler’s Gorge na miradi mingine inayoendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tunachokiona hapa ni kitu kimoja; wenzetu wameshaona Messi wa CCM ni Mheshimiwa Dkt. Magufuli. Kwa hiyo, ni lazima mshikeshike miguu. Wana-CCM lazima tukae tayari kumlinda Messi wetu asiumizwe, asilete madhara katika mambo hayo. Kwa hiyo, nafikiri kwamba haya ni mambo ya msingi ya kufanya, lakini naomba Wizara zinazohusika ziangalie Jimbo la Bunda. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.