Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017.

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017.

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Joseph Pombe Magufuli kwa uongozi wake wa kuwathamini wananchi kwa maendeleo yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Serikali kuona inapunguza gharama ya uzalishaji wa umeme kwa kutumia mafuta, kama ilivyo mikoa kadhaa ya nchi ikiwemo Mkoa wa Rukwa, Katavvi na kadhalika. Tunaomba kuunganishwa na gridi ya Taifa kwa sasa takribani mikoa yote. Mfano Rukwa tunatumia mafuta na umeme wa kutoka Zambia. Hii harakati ya kuanzisha viwanda tunahitajika kuwa na umeme wa kutosha na kukidhi haja.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mikoa ya Kusini kuna nafaka za kutosha, tunahitaji kuziongeza thamani, hivyo umeme ni muhimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia umeme REA III ufikishwe kwenye vijiji na vitongoji vyote nchini, kwa hatua ya sasa, ikamilishwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuunga hoja mkono.