Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017.

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017.

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchangia katika hoja hii kama ifuatavyo:-

Kwanza, naipongeza Kamati kwa ufuatiliaji wa miradi mbalimbali na kwa ripoti nzuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, bei za gesi ziko juu sana mpaka wananchi wanashindwa kununua gesi hiyo. Naomba Serikali ione ni namna gani bei zinapungua na kuwawezesha kununua kwa bei nafuu. Kwa namna nyingine watu wataendelea kuharibu mazingira kwa kukata miti hovyo kwa ajili ya kutengeneza mkaa na kutumia kuni kwa ajili ya kupikia.

Mheshimiwa Naibu Spika, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO); nashukuru Serikali inajitahidi kupeleka umeme hadi vijijini, lakini kuna tatizo limezuka la kukatika umeme kila mara. Mfano, Mjini Njombe na baadhi ya maeneo hapa Dodoma hasa eneo la Kisasa umeme unakatika mara kwa mara.

Mheshimiwa Naibu Spika, naiomba Serikali ione namna gani inarekebisha miundombinu ya umeme ili usikatike mara kwa mara, iimarishe miundombinu kama transformer na nguzo na waya wa muda mrefu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC); bei za mafuta zinapanda kila kukicha hii inatokana na kuwa tunategemea kutoka nje maana sisi hatuna matanki kwa ajili ya kuhifadhi mafuta hayo. Naiomba Serikali iweke matanki yake kwa ajili ya kuhifadhi mafuta haya ili bei ishuke.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ina madeni TANESCO; hii inasababisha uendeshaji unakuwa mgumu na Shirika limekuwa likijiendesha kwa hasara. Serikali iwachukulie hatua watu wenye madeni sugu lakini pia Serikali yenyewe ilipe madeni yake

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.