Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa hii nafasi ya kipekee nami niweze kuchangia hizi Kamati mbili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kuzipongeza Kamati zote mbili zimeleta ripoti zao nzuri na mapendekezo mazuri sana ambayo nina imani kama yakifanyiwa kazi na Serikali tunaweza kwenda kwenye hatua nyingine ambayo ni nzuri zaidi kimkakati kwenye mambo ya kilimo na ardhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ilivyoeleza taarifa ya Kamati ya Kilimo nafikiri na jinsi walivyoongelea wenzangu, tuna changamoto kubwa sana kwenye sekta hii ya kilimo hasa ukizingatia kuwa kilimo ndiyo sehemu kubwa inayoajiri Watanzania zaidi ya asilimia 75, lakini kwa kiasi kikubwa hatuoni mikakati madhubuti kabisa inayochukuliwa ukilinganisha na umuhimu wa sekta hii ya kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano mdogo kule kwangu katika Halmashari ya Mbeya tunalima pareto na zao hili lina umuhimu wa kipekee sana duniani. Halmashauri yetu tunaongoza kwa kilimo cha pareto Tanzania. Bahari nzuri kwa pareto ile inayolimwa kule vilevile inaongoza kwa
uzalishaji kwa Bara zima la Afrika. Pareto inayolimwa kwenye Halmashauri ya Mbeya na sisi ni namba mbili katika uzalishaji wa pareto duniani, lakini huwezi kuona mahali popote katika makaratasi ambapo limeupa umuhimu wa kipekee hili zao la pareto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumshukuru Waziri pamoja na Naibu Waziri wamechukua hatua ambazo kidogo zinaanza kuonesha mwanga wa kwamba labda hili zao nalo linaweza kuwaletea manufaa Watanzania. Kwa kipekee kabisa Naibu Waziri alitembelea Jimbo langu, akakutana na wakulima, akaona wakulima wanavyopata tabu ya soko la pareto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo kubwa la pareto hii ni monopoly. Tuna mnunuzi mmoja tu anayenunua zao hili na kwa bahati mbaya mnunuzi huyu katika mnyororo wa zao la pareto yeye ana-control kutoka kwa mkulima, uzalishaji na mpaka soko la dunia kwa vile kwenye soko la dunia nako amelikamata yeye.

Mheshimiwa Mwenyekiti, shida tunayoipata ni kwamba yeye sasa ndiyo atampangia mkulima bei na kwa bahati mbaya hana huruma na mkulima na Tanzania. Kwa bei ya mkulima ni Sh.2,300 kwa kilo lakini kwa bei ya pareto hiyo hiyo ni Sh.8,000 kwa kilo anayouzia yeye sasa angalia hiyo spread, angalia ni kiasi gani katika dunia ya leo mkulima ananyonywa kiasi hiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, pendekezo la langu, Kamati iongeze katika taarifa yake mapendekezo kuwa Serikali iweke mkakati wa kipekee kuangalia ni namna gani zao hili la pareto litakuwa na manufaa kwa wananchi. Vilevile huu uzalishaji wa pareto badala ya hii kampuni kupeleka crude extract na powder ya pareto waweze kutengeneza finished product ambazo zinaweza kuuzwa na zikapata jina ya kwamba hii pareto inatoka Tanzania. Tumenyonywa kwa kiasi kikubwa nafikiri hii itaweza kutusaidia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi tunazungumzia Tanzania ya viwanda, nafikiri Serikali iweke mkakati namna gani tuwe na viwanda vidogo vidogo kwa ajili ya kuchakata hayo mazao ikiwemo pareto. Kiwanda cha Pareto kinahitaji mtaji wa dola laki moja na nusu tu ambazo ni karibu milioni 300. Nafikiri hizi kwa kiasi kikubwa kama kweli tuna nia nzuri ya kukiendeleza kilimo, tunaweza tukaanzia kwenye pareto tukawa na viwanda vingi na tukawasaidia wakulima waweze kupata faida. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiachilia mbali pareto, kwa kiasi kikubwa mwaka huu tumepata matatizo sana kwenye mazao na hasa zao la mahindi. Serikali ilikuwa imepiga marufuku kupeleka mahindi nje ya nchi. Matokeo yake leo hii mahindi kwenye soko letu la Mbeya yameteremka bei kutoka Sh.12,000 mpaka Sh.5,000 kwa debe, leo hii linauzwa kwa Sh.3,800.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa fikiria mkulima amepata hasara ya namna gani na hata hii Sh.3,800 huwezi kupata mnunuzi. Masoko ya huko nje tuliyozuia wenzetu wame-take advantage wamepeleka mahindi kutoka Zambia, Malawi na South Africa yamejaa kwenye yale masoko tuliyokuwa tunapaleka sisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafikiri tujaribu kujitathmini na kuangalia kama hizi taarifa tunazozipata kwa wataalam wetu zinatusaidia katika ku-make decision. Nafikiri tunawaumiza wakulima na tukiumiza wakulima kwa kiasi kikubwa tunawaumiza Watanzania walio wengi ambao wanategemea kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile napenda kutoa pendekezo langu na kuiunga mkono taarifa ya Kamati ya Maji kuwa Serikali iweke mkazo tuanzishe Wakala wa Maji Vijijini kwa sababu kwenye Halmashauri zetu tuna tatizo kubwa, hatuna wataalam wa maji, tuna mainjinia na kadhalika lakini uwezo wao wa kusimamia miradi hii mkubwa ya maji ni mdogo sana. Ni afadhali tuweke chombo cha wataalam kusaidia kuhakikisha kuwa Watanzania wanapata maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, Mbeya tuna maji mengi sana lakini toka 2013 hakuna mradi hata mmoja wa maji uliokamilika licha ya bajeti kubwa ya Serikali tuliyoletewa. Nina imani kuwa Wakala wa Maji atutasaidia kama tulivyoona kwenye REA na barabara. Kwa hiyo, naungana na Kamati wahakikishe kuwa hiki chombo kinaanzishwa...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)