Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwanza nianze kusema kwamba naunga mkono taarifa za Kamati zote mbili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba ninukuu Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2015 mpaka 2020, inasema: “Katika kipindi cha miaka mitano, Chama cha Mapinduzi kitaweka kipaumbele cha kuhakikisha kuwa kilimo nchini kinakuwa endelevu na chenye tija ili kuwezesha Taifa kujitosheleza kwa chakula, kuongeza mapato ya wakulima, kuwa chanzo cha kuaminika cha mapato.” Hii ndiyo ahadi yetu kwa wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mawaziri wanapoapa mbele ya Mheshimiwa Rais, katika kiapo chao wanasema watamshauri Mheshimiwa Rais. Tunapochagua Rais na Wabunge na inapoundwa Serikali inaenda kutekeleza Ilani ya Uchaguzi wa Chama cha Mapinduzi. Humu ndani huwa Wabunge tunagawanyika, tunaotetea wafugaji, tunaotetea wakulima. Nataka niwaambie, hii ni divide and rule. Asilimia 70 ya wakulima wa nchi hii, asilimia 80 ya hii docket inafanya kazi ya kilimo na mifugo. Kwa hiyo, anapoathirika mfugaji ndivyo hivyo anavyoathirika mkulima. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nikupe jambo hili dogo tu; Bajeti ya mwaka 2010/2011 asilimia 7.8 ndiyo ilikuwa bajeti ya kilimo; Bajeti ya 2012 asilimia 6.9 ndiyo ilikuwa bajeti ya kilimo; Bajeti ya 2016/2017 asilimia 4.9 ndiyo bajeti ya kilimo. Angalieni namna gani tunavyo-lose focus. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye mipango ya matumizi ya ardhi tumeweka maeneo kwa ajili ya misitu, maeneo kwa ajili ya game reserves, maeneo kwa ajili ya wanyama, lakini ukija kuna ardhi ya vijiji ambayo imepangiwa matumizi haizidi asilimia 30. Pia tunazo ardhi za miji. Nataka niulize leo, Mawaziri hapa watuambie, ni lini wamekaa chini kuja na master plan ya ku-allocate ardhi kwa ajili ya wafugaji na wakulima ili tuweze kujua namna gani tunawapanga watu wetu? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tembo akila mahindi, akiua mtu, kuna kafidia na tembo anaheshimiwa kweli, lakini mwananchi akilima ndani ya reserve ya wanyamapori, ataadhibiwa kwa faini. Akivuna mazao yake, anaambiwa asiuze ili tuweze kudhibiti mfumuko wa bei. Tunatengeneza artificial control mechanisms za kuonyesha uchumi wetu uko vizuri, wakati tunawatia watu umaskini. This is unfair. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi nataka niseme kwa Waheshimiwa Wabunge wenzangu wa Chama cha Mapinduzi, we are not fair kwa wakulima, kwa wafugaji, kwa wavuvi, na kwa wamachinga. Who are we expecting kesho kwenda kumwomba kura? Tusikubali kuingia kwenye record ya kukipeleka chama chetu kubovu kwa makosa ya Mawaziri Serikalini. We should not allow kuwatia umaskini Watanzania. Tusiruhusu kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo mahindi yanazalishwa tena…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)