Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Yosepher Ferdinand Komba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. YOSEPHER F. KOMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mapango ya Amboni ni moja ya vivutio vikuu vya utalii katika Jiji la Tanga. Ni mapango ambayo ni muhimu sana kwa mapato na mvuto kwa Jiji la Tanga , lakini kuna changamoto zifuatazo:-

(i) Miundo mbinu ya barabara kwenda mapangoni;

(ii) Mto unaopita pembezoni unamega kingo za mapango; na

(iii) Uchimbaji wa kokoto unaharibu mazingira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri kwamba Mpango mkakati na wa haraka na dharura ili kuboresha miundombinu yote muhimu ili kuongeza mapato; Eneo la mapango liainishwe ili liweze kutunzwa na kulindwa; Vivutio vingine kama Chemichemi ya Maji moto ya Sulphur Amboni, Mapango ya Tongoni na vivutio vingine ili kuvitangaza na kuviboresha zaidi; na Serikali ifuatilie na kuvitangaza vivutio ambavyo ni vya kipekee kama vile Msitu wa Asili wa Amani na Vipepeo adimu duniani ambavyo vinapatikana huko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mipaka katika hifadhi; kumekuwa na migogoro mingi na ya muda mrefu kati ya wananchi wanaoishi karibu na hifadhi na Serikali au wahifadhi wa maeneo yaliyotengwa kwa hifadhi. Kumekuwa na mgogoro mkubwa kwa wananchi wanaoishi Kata ya Lunguza kwenye mbuga ya Mkomazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu ni kwamba Serikali ikapime mipaka upya ili kuondoa migogoro; Katika kupima waweke free zone ili kupunguza migogoro na ukaribu wa makazi ya wananchi na hifadhi; Hifadhi zijitahidi na zisimamiwe ili zirejeshe kiasi cha mapato katika miradi ya kijamii ili kusaidia kuwajengea wananchi imani na nia njema ya kuwa na hifadhi ni kwa maendeleo yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na naomba kuwasilisha.