Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Jitu Vrajlal Soni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie taarifa ya Kamati ya kwanza kwa kuwapongeza sana kwa kazi nzuri na kubwa wanayofanya. Naomba nishauri Bunge iangalie namna ya kuwa na mfumo wa Kamati za Kudumu kufanya kazi ya pamoja coordination, uratibu baina ya Kamati mbalimbali kwenye masuala mtambuka. Kwa sasa kila Kamati inajitegemea na sio rahisi kufanya kazi ya pamoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia niendelee kushauri Kamati ichukulie kwa umuhimu suala la kulinda ardhi za kilimo, mifugo na pia maeneo ya uvuvi zisibadilishwe matumizi kiholela na pawe na sheria itakayowezesha Bunge kuridhia kubadilishwa matumizi ya ardhi hasa za kilimo, mifugo na uvuvi. Leo hii nyingi zenye rutuba za kilimo zimegeuzwa kuwa makazi, viwanda na matumizi mengine. Pia kuishauri Serikali kutatua mgogoro wa ardhi baina ya Hifadhi mbalimbali na wakulima, wafugaji na hata ushoroba mbalimbali zinapovamiwa ambazo ni muhimu kwa uendelevu wa hifadhi zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ningeshauri tuangalie namna ya kuchangia kuboresha misitu na hifadhi zetu ili mchango wake uwe endelevu kwa Taifa letu. Ni vyema mapato yanayotokana na maliasili sehemu yake mfano asilimia 10% yarudishwe kuboresha mazingira. Kwenye kufanya
uratibu na Kamati zingine tuishauri Serikali kuangalia kilimo, hifadhi, kulinda vyanzo vya maji na pia kuzuia mmomonyoko wa udongo kwenda kwenye maziwa. Sheria zipo ila hamna ufuatiliaji na usimamizi wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba Kamati ikubali kufanya utaratibu wa karibu na Kamati zingine na kupokea maoni ya Wabunge na wadau wengine ili kuboresha utalii. Tumejaliwa na Mwenyezi Mungu kupata vivutio vingi vya aina mbalimbali lakini hatujafikiria hata asilimia 10% kufaidi rasilimali tuliyonayo. Tunashauri tuangalie mfumo wa kuishauri Serikali namna ya kufuatilia na kusimamia sheria zilizopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, Kamati pia iweze kushirikiana na taasisi ya Wabunge uliopo Bungeni ya TAPAFE ili kuendelea kupata tija. Ahsante.