Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa hii haikuangazia utekelezaji wa Dhana ya Hifadhi za Jamii (WMA). Nilitegemea kupata taarifa kuhusu idadi ya WMAs zilizosajiliwa tangu dhana hii ianzishwe chini ya Sera ya Wanyamapori mwaka 2003 hadi sasa (miaka 15) na manufaa ya kiekolojia na uchumi yaliyopatikana. Jamii zenye WMA zimefaidikaje? Serikali imefaidikaje? Serikali ina mkakati gani kuendeleza dhana ya WMAs na WMAs ngapi zinatarajiwa kuanzishwa zaidi katika nchi yetu?