Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kuunga mkono mapendekezo ya Kamati hii, naomba kusisitiza kwamba migogoro ya ardhi hasa vijijini imezidi kuongezeka siku hadi siku. Kutopimwa ardhi kumesababisha miingiliano na vurugu kubwa hasa ikizingatiwa kwamba maeneo mengi ya vijijini hayajapangiwa matumizi bora ya ardhi zao, kwa mfano, Jimboni kwangu Same Mashariki, wakulima na wafugaji na TANAPA (Mkomazi National Park).

Mheshimiwa Mwenyekiti, mgogoro wa wanyamapori kuingia kwenye mashamba na makazi ya wananchi umeongeza umaskini Jimboni kwangu. Mazao ya wakulima yamekuwa yakiharibiwa sana na wanyamapori. Wananchi wengine wameumizwa na wanyama hao. Badala ya kulipwa fidia, wananchi wamekuwa wakipewa kifuta jasho ambacho sio sawa na madhara waliyopata. Wanyamapori wamekuwa wakithaminiwa kuliko wananchi. Matokeo yake wananchi hawaoni faida ya kuwa na mbuga za wanyama katika maeneo yao. Nashauri Wizara hii ya Maliasili na Utalii ikishirikiana na Wizara ya Ardhi iweke utaratibu mzuri utakaoondoa matatizo haya ya wananchi.