Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nipongeze uwasilishaji wa taarifa ya Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii. Napenda kuishauri Serikali kama ifutavyo:-

(i) Ipunguze mlolongo wa tozo kwenye utalii kwani umesababisha watalii wengi kushindwa kuja Tanzania hivyo kupunguza pato la Tanzania;

(ii) Iboreshe hoteli zetu za kitalii na huduma ziwe za kisasa na pia kutoa elimu kwa wahudumu wetu jinsi ya kuwahudumia watalii wetu. Vilevile iboreshe mitaala ya ufundishaji wahudumu wetu kwani wamekuwa hawakidhi kiwango cha kimataifa hivyo watalii wengi kutofurahia huduma zetu wawapo nchini.

(iii) Ishughulikie migogoro ya ardhi ambayo mingi inasababishwa na Maafisa Ardhi katika Halmashauri kwa kupima maeneo ya wananchi na kushindwa kulipa fidia na kuuza viwanja hivyo kama vyanzo vya mapato ya Halmashauri wananchi wakiachwa bila kipato chochote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri kuwa wanapogawa viwanja vilivyopimwa wazingatie kaya au nyumba husika ina vijana wangapi wenye uwezo wa kujiajiri ili kuondoa tatizo la vijana kukosa ardhi kwa ajili ya kujiajiri.

(iv) Iwakemee viongozi ambao ni Watendaji wa Kata na Vijiji wanaouza ardhi za vijiji bila kushirikisha wananchi.

(v) Itoe elimu kwa wananchi juu ya haki ya msingi ya ardhi na jinsi ya kumiliki ardhi. Niombe pia kuondoa urasimu wa upatikanaji hati miliki kwenye ofisi za ardhi.

(vi) Iharakishe urasimishaji wa ardhi ili wananchi waweze kutumia ardhi hiyo kwa ajili ya kujipatia mikopo ya kilimo.

(vii) Ishughulikie mgogoro uliopo kati ya Halmashauri ya Kibaha na wananchi wa Lumumba na Mwanangali ambao umepelekea wananchi kuwa maskini na kushindwa kuendeleza maeneo yao kwa miaka kumi.