Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Suzana Chogisasi Mgonukulima

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. SUZANA C. MGONOKULIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Taifa letu la Tanzania sekta ya kilimo inaajiri wananchi asilimia 70 lakini bado Serikali haiwekezi kiasi ambacho kitakuwa na uwiano na hitaji la sekta hiyo.

(i) Pembejeo haziji kwa wakati na za kutosha mahitaji.

(ii) Wataalam wa sekta hiyo wapo wa kutosha katika Halmashauri.

(iii) Bei ya mbolea si rafiki kwa wakulima hasa kwa mwaka 2017 - 2018, bei ya mahindi iko chini sana kuliko bei ya mbolea. Gunia la mahindi ni Sh.30,000 wakati mfuko mmoja wa mbolea ya UREA ni Sh.56,000.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mifugo katika Taifa letu la Tanzania imekuwa tatizo kubwa kwa wafugaji kwa kukosa maeneo ya kufugia. Serikali iwe na mkakati wa makusudi kuhakikisha wakulima na wafugaji wametengewa maeneo kwa shughuli za kilimo na mifugo ili azma ya Tanzania ya viwanda iwezekane. Viwanda vinavyotakiwa kuwepo vinahitaji malighafi kutokana na kilimo na mifugo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu uvuvi, matatizo ya Sheria ya Uvuvi itazamwe kwa macho ya faida ya wavuvi na Taifa, siyo kuchoma nyavu za wavuvi bila kuhakikisha vyavu hii ni zile zinazotakiwa au la hasha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali bajeti inayopitishwa na Bunge ifike kwa wakati kwenye Wizara husika.