Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Mwenyekiti, Kampeni ya kuchoma kambi, kuvunjwa mitumbwi na kuchoma nyasi, haiwezi kuandoa uvuvi haramu kwa sababu mwisho wa siku itatengeneza maskini wengi ambao maisha yao yote ni uvuvi na watavua kwa sumu au njia mbaya zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kampeni ya kukata nyavu kutoka double triple kuwa single, haijafanyiwa utafiti, Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika vina vyake haviko sawa. Ukiwafanya wavuvi wote kutega single watavua kwenye mazalia ya samaki na iwapo itakuwa hivyo zoezi lote hili ni kupoteza muda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Nyavu ya single; iwapo itatumika maji marefu ile ya nchi 7", 8", 10" inaweza kukamata samaki wa robo kilo, kilo moja mpaka kilo 100. Utaratibu wa kupiga watu faini ovyo ni sawa na kuwaagiza wavuvi kutupa samaki kwenye maji kwa sababu samaki akinasa hufa pale pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nyavu ya single; haiwezi kuvua maji marefu kwa sababu nyavu ina kina cha mita nne wakati ziwa lina kina cha mita 84.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu faini, zitumike sheria za uvuvi siyo sheria za mazingira kupambana na wavuvi.