Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia kuhusu uvuvi haramu. Tunapata matatizo makubwa kama nchi kuhusu nyavu za kuvulia ambazo si rafiki kwa samaki zinazopelekea kuzaliwa uvuvi haramu. Niende mbele zaidi kwa kusema nyavu hizi ambazo si rafiki kwa samaki ni mara nyingi zinakamatwa na kuteketezwa lakini tatizo hili la nyavu haramu halijapata kamwe kupungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niishauri Serikali kwa kuwa wananchi wetu wanazipenda sana hizi nyavu na kupelekea wao kuingia hasara za mamilioni ya fedha kwani pindi wanapokamatwa zinateketezwa na kwa kuwa hawakomi wanaendelea kuzitumia kinyume na maelekezo ya Serikali. Basi sasa ni vyema Serikali yenyewe ichukue jukumu la kuingiza nchini nyavu za kuvulia na pia Serikali ichukue jukumu la kumiliki viwanda vya kutengeneza nyavu ili tuondokane na kuteketeza nyavu hizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nyavu zinazoteketezwa ambazo ni haramu tunateketeza mabilioni ya fedha za wavuvi ambao ni Watanzania tunavuruga uchumi wa nchi.

Namalizia kwa kusema nyavu za kuvulia ziwe chini ya Serikali yenyewe, Serikali ihusike na utengenezaji na uagizwaji wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.