Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, wakulima walipata ari ya kujihusisha katika kilimo hususan kilimo cha mahindi na alizeti katika Mkoa wa Iringa japo gharama za pembejeo ni ghali na wakafanikiwa kupata mazao hayo kwa wingi. Kitu cha kushangaza ni kutolewa kwa maagizo toka Serikalini ya zuio au uuzaji mazao yao hasa mahindi nje ya nchi na kuathiri wakulima hao kujipatia kipato.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali iweze kuruhusu wakulima hao kufanya biashara hiyo ya kutafuta namna ya kuwafanya wakulima hawa waweze kuendelea na kilimo kwani zuio hilo limeshusha bei ya mahindi hadi kufikia sh.6000 kwa debe moja gharama ambayo haitoshelezi hata ununuzi wa mfuko mmoja wa mbolea kwa gunia moja la mahindi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Iringa wanashughulika pia na kilimo cha nyanya na mbogamboga. Changamoto kubwa katika kilimo hiki ni ukosefu wa elimu hasa kwa wakulima kuhusu kilimo cha kisasa. Hii husababisha uzalishaji mdogo usio bora kwa zao hilo. Aidha, changamoto ya pembejeo na magonjwa ya nyanya, Serikali itoe elimu ya kilimo cha mazao haya na iyape kipaumbele. Itengwe bajeti ya kutosha kuwezesha shughuli za tafiti kwa ajili ya namna ya kutibu magonjwa ya nyanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Benki ya Maendeleo ya Kilimo. Wakulima walio wengi wanashindwa kukuza kilimo kwa kukosa mitaji. Benki ya Kilimo, (TADB) iliomba shilingi bilioni 800 lakini hadi Desemba, 2017 walikuwa na mtaji wa bilioni 66.7 tu. Hivi ukijiuliza watawafikia wananchi wangapi kwa fedha hiyo tu? Naishauri Serikali iweke msisitizo katika upelekaji wa fedha katika benki hiyo kwani itawafikia wakulima walio wengi na kusaidia kupunguza umaskini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo cha umwagiliaji. Serikali iweze kutoa kipaumbele katika kilimo cha umwagiliaji kwani ndio utatuzi hasa pale ambapo kunakuwa na uhaba wa mvua. Ni asilimia ndogo sana inatumika kwa kilimo hiki, Serikali ikiweza kujenga mabwawa ya kutosha kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja ya Kamati.