Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Abdallah Ally Mtolea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Temeke

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuongelea kuhusu suala la makokora. Zoezi la uchomaji moto nyavu za asili zenye macho madogo madogo linaathiri uchumi wa wavuvi wa dagaa ambao hawana uwezo wa kununua nyavu maalum za macho madogo za kuvulia dagaa. Serikali iwatambue wavuvi wa dagaa na iwasaidie kuwapatia nyavu hizo ili waepuke kutumia makokora badala ya kutumia mabavu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile niongelee suala la kuzuia usafirishaji wa viumbe hai. Sasa ni zaidi ya miaka miwili toka Serikali izuie usafirishaji wa viumbe hai kama mijusi, panzi na kadhalika. Zoezi hili linawaumiza wajasiriamali wa shughuli hizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.