Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Dr. Charles John Tizeba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kutupa nafasi kutoa maelezo kuhusu hoja ambazo zimetolewa na Kamati na Wabunge ambao wamechangia taarifa za Kamati zilizowasilishwa leo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuishukuru sana Kamati yetu kwamba tumefanya kazi kwa ushirikiano mkubwa sana, wametushauri mambo mengi na katika ushauri wao yako ambayo tuliyaacha na tukachukua ushauri kuufanyia kazi. Kwa hiyo, katika mapendekezo yaliyotolewa na Kamati kimsingi yote yanakubalika na tutaenda kuyafanyia kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, labda nizungumzie mambo manne na kama muda utatosha nitazungumzia na lingine la tano, lakini nataka nizungumzie suala la masoko ya mazao, lakini pia tunavyokabiliana na wadudu na visumbufu vya mimea, jambo la uagizaji wa mbolea kwa pamoja na tatizo la uchakachuaji wa korosho iliyosafirishwa nje ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na tatizo la masoko ya mazao. Nimewasikiliza kwa uzuri sana Waheshimiwa Wabunge waliozungumzia ukosefu wa soko la mazao hasa mahindi na mbaazi. Lakini pia nimemsikia Mheshimiwa Maige akizungumzia suala la ukosefu wa soko la tumbaku.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli haya mazao kama yalivyo mazao mengine ambayo pia hayakuzungumziwa hapa ndani. Masoko yake siyo mazuri sana. Na masoko haya siyo mazuri kwa mazao yanayozalishwa Tanzania tu, labda hili ndiyo naomba tuelewane vizuri. Ni hata wazalishaji walio nje ya Tanzania wanakabiliwa na tatizo hili hili la masoko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati Tanzania mahindi yameshuka bei mpaka shilingi 5,000 kwa debe, jirani zetu Zambia debe la mahindi liko shilingi 2,600; Malawi debe liko shilingi 3,100. Mwaka juzi mahindi yalipanda bei sana kwa sababu nchi zote zilizotuzunguka hawakuwa na uzalishaji kwa hivyo soko likabaki chanzo cha mahindi kikabaki ni Tanzania peke yake.

Kwa hiyo, suala sasa hivi la uwezekano wa kupandisha bei ya mahindi wakati majirani zetu wote wanayo mahindi yanayowatosha halipo. Misimu inatofautiana, kwa hiyo wanavyozalisha na wao hawawi tena na sababu ya kuja kwetu ndivyo hivyo hivyo ilivyotokea kwa mbaazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, traditional soko la mbaazi la Tanzania ilikuwa ni India na wazalishaji wameendelea kuzalisha na wakiuza huko India miaka yote.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa suala la Waziri Mkuu wa India alipokuja hapa akazungumza yes watu waliamasika wakazalisha zaidi na kwa sababu bei ya msimu iliyotangulia ilikuwa kubwa uzalishaji ukaongezeka watu wakaenda benki, wakachukua pesa ili wazalishe mbaazi kwa ahadi kwamba watapata soko la uhakika ambalo wamelizoea, India imezuia. Kwa hiyo, soko la mbaazi la India limesabaisha ku-distort soko la mbaazi la ndani ya Tanzania, na hapa namshukuru sana Mheshimiwa Mgumba amelieleza vizuri tatizo la commodities zile, lakini pia nimfahamishe kwamba nchi ya India walisaini mkataba na Mozambique wa kununua mbaazi sisi waka-deal dull kumbe wakichungulia uzalishaji wao.

Mheshimiwa Naibu Spika, uzalishaji wao ulipokuwa mzuri kuliko walivyotarajia wakaweka mguu chini hawakutaka kusaini mkataba wa makubaliano na kule Mozambique ambako waliingia mkataba wamenunua tani 135,000 ya mbaazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo masoko ya mazao twende kwenye tumbaku, tumbaku inazalishwa kwa mkataba.

Tumbaku inazalishwa kwa mkataba, baada ya mabishano ya bei kwenye Tobacco Council...

T A A R I F A . . .

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa ya Mheshimwia Gekul sijui niikatae kwa sababu bila maelezo ya kilichotokea tutazungumza nini hapa. Sidhani kama hata ni utaratibu mzuri, lakini anyway ndiyo Bunge lenyewe lilivyo. Kwa hiyo, masoko haya...

T A A R I F A . . .

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni suala tu la uelewa kwa sababu ukielewa kwamba tuna misimu tofauti na kwa hiyo sisi uzalishaji wetu unatangulia na wengine unafuata huwezi ukaacha mahali ambako soko la ndani haliko regulated kwa sababu ya nanilii... Historia ya mwaka jana nadhani iko bado live kabisa kwenye vichwa vya Wabunge. Tulienda tukakubaliana kwamba tuache mahindi yaende nje baada ya miezi miwili Bunge hili hili ndiyo likaanza kusema kwamba…

T A A R I F A . . .

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwambie tu Mheshimiwa Mwakajoka kwamba utafiti tunafanya na utafiti tuliokwishaufanya hatua tutakazochukua mwaka huu zitakuwa tofauti sana na hatua ambazo tumekuwa tumechukua miaka ya nyuma.

Mheshimiwa Mwenyekiti kwa hiyo, utafiti tulioufanya tutachukua hatua tofauti na hizi ambazo zinatufikisha kuvutana na Serikali na Wabunge. Soko la kahawa la Tanzania limeendelea kuwa duni kwa sababu ya mazingira ya kodi ambayo tunayo Tanzania ukilinganisha na nchi zinazozalisha kahawa…

KUHUSU UTARATIBU . . .

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nasikitika tu kwamba Mheshimiwa Heche anasema nimepotosha Bunge, ninachokisema ni ukweli na ukweli huu kama haumpendezeshi masikio bahati mbaya. Mazao haya yana sheria iliyotungwa na Bunge. Kwa hiyo, hatuwezi tukaicha sheria tukaenda na mambo ambayo hayana utaratibu. Kupeleka tumbaku Kenya kuna hitaji utaratibu wa sheria, utoroshaji wa tumbaku ni uvunjaji wa sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nilikuwa nazungumzia habari ya masoko ya mazao, commodity markets ziko volatile dunia nzima na siyo Tanzania peke yake kwa hiyo ikitokea hizi fluctuation za bei fluctuation za nini siyo kwa sababu nchi hii ni Tanzania, hili ni jambo ambalo sasa hivi lina affect dunia nzima uliza nchi yoyote bei za mazao zimeporomoka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie tunavyokabiliana na wadudu. Ni kweli suala la worms lilijitokeza mwaka jana na sisi tulitoa taarifa kwa umma namna ya kuwatambua na namna ya kudhibiti wadudu hawa. Bahati mbaya sana wadudu hawa wamekuwa wanafanana na wale viwavijeshi tuliowazoea, kwa hiyo, watu wakadhani kwamba wataporomwosha tu na mvua ikinyesha, hawakuchukua hatua. Serikali ilichukua hatua ya kupita mikoa yote ambayo ilikwishaonekana wadudu hawa wapo, kutoa mafunzo na kuelekeza wananchi namna ya kukabiliana na ...worms, lakini wameendelea kuzaana hivi hivi. Sasa hivi kuanzia wiki wiki hii tutapeleka dawa kwenye Halmashauri ambazo Mikoa yote imekuwa-affected na hawa wadudu ili halmashauri zigawe hizi dawa kwa Wananchi wapulize kwenye mashamba yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna tatizo liko kwenye pamba kuna wadudu, funza na utitiri, wamekuwa wanashambulia pamba lakini tuseme tuu kwamba dawa imekwishapatikana fedha tuliyokuwa tunahitaji tumepata dawa imenunuliwa inaendelea kusambazwa na Bodi ya Pamba, nilikuwa huko mwenyewe jana, kwa hiyo, tatizo hili nalo tutakabiliana nalo kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, leo wale kwelea kwelea wanaoharibu mazao Shinyanga na Simiyu, upuliziaji kwa ndege utaanza lakini pia dawa kwa ajili ya panya walioko kwenye maeneo ya Handeni, Morogoro, Ifakara, Mlimba na Chalinze na kwenyewe dawa imepatikana tutapeleka kule, ili Halmashauri zikasimamie uteketezaji wa hawa panya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie kidogo suala la mfumo wa uagizaji wa mbolea kwa pamoja. Huu mfumo una tatizo la msingi la kwamba unanyang’anya faida kwa baadhi ya wafanyabiashara waliozoea kupata faida kubwa. Kwa hiyo, lazima yatengenezwe mazingira ya kuonesha kwamba mfumo huu haufanyi kazi vizuri na sisi tunachokifanya ni kukabiliana na hayo ambayo yanajitokeza, wakati tunatekeleza mfumo wenyewe.

Mheshimiwa Mwenyekti, Kamati imesema kwamba lengo halikufikiwa; jibu ni ndiyo na hapana kwa sababu yako maeneo ambayo bei ilikuwa kubwa sana mbolea tuliyoiagiza kwa ile awamu ya kwanza ilikuwa ya bei ya chini kulinganisha na bei iliyokuwapo kwenye maeneo hayo. Sasa hivi bei ya Urea imepanda katika soko la dunia hatuzalishi wenyewe Urea hapa kwa hivyo awamu ya pili ilipoagizwa imekutana na bei iliyopanda. Hata hivyo, control tunazoziweka ndio zinatuhakikishia kwamba mkulima hatauziwa kwa bei ya kinyang’anyi, tunaweka mechanisim ambayo itamhakikishia mkulima ananunua kwa bei himilivu, tukiacha hivi hivi ndio mfuko unakwenda mpaka shilingi 80,000; 90,000.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo suala la BPS limekutana na changamoto ya ufikishaji wa mbolea kwenye maeneo ya vijijini ambako miundombinu ya barabara iliharibika usafirishaji ukapanda bei. Kwa hiyo, wafanyabiashara wakawa wanashindwa kusafirisha na kuuza kwa bei elekezi na sisi tulichukua hatua mara moja tukawaambia kuwa mikoa wafanye tathmini ya gharama halisi ili waweze ku-adjust gharama za kutoka kwenye Wilaya kwenda huko vijijini na jambo hilo limefanyika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho, ni habari ya korosho na uchakachuaji uliotokea. Taarifa tulizonazo, tatizo katika korosho halikuanza mwaka huu, limeanza mwaka jana kwa wafanyabiashara wa kutoka Vietnam.
Uchakachuaji…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)