Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Ester Michael Mmasi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. ESTER M. MMASI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa fursa hii na mimi niweze kuchangia mchango wangu mdogo kulingana na uwasilishwaji wa Taarifa ya Kamati ya Sheria Ndogo, lakini pia na uwasilishwaji wa Kamati ya Sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijaenda mbali napenda kuipongeza Ofisi ya Waziri Mkuu chini ya uongozi wa Mheshimiwa Jenista Mhagama pamoja na Mheshimiwa Mavunde kwa kazi yao nzuri ya kuweza kufanya majukumu yao yakawa na tija hata kwa sisi Wanakamati wa Sheria Ndogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi Wajumbe wa Kamati ya Sheria Ndogo tulikuwa na malalamiko mengi ya muda mrefu. Na malalamiko yetu yalikuwa ni Ofisi ya Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina furaha ya pekee kusimama katika Bunge lako hili Tukufu kutoa pongezi za dhati kwa Ofisi ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, kwa kweli wameutendea haki mhimili huu wa sheria. Ninaomba jambo moja lifanyike. Ni dhahiri kwamba tumempata Mpiga Chapa wa Serikali ambaye anakaimu kwa nafasi yake, Bwana Kaswalala. Bwana Kaswalala amefanya mambo mengi, ameleta reforms nyingi, ametengeneza retantion strategies, lakini ameleta mabadiliko kwa muda mfupi sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bwana Kaswalala mpaka leo anakaimu. Hata hivyo pamoja na suala hili la kukaimu ambalo tumeona kimantiki halileti tija kwa mtu ambaye tunamuona ana uwezo katika nafasi hii tukashindwa kum- confirm. Kwa hiyo, ni ombi langu kwa Wizara hii, ni ombi langu kwa Ofisi hii tuweze kum-confirm Bwana Kaswalala kwa sababu ukiangalia Sheria za Utumishi wa Umma provision ni three months tofauti na hapo mtu ame-qualify tunampa nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala zima la mitambo mibovu kwa Ofisi ya Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali. Tukipata mitambo imara ndio namna pekee ya kuweza kutunza siri na kuhifadi nyaraka za Serikali. Tunaiomba ofisi husika iweze kumsaidia Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali ili aweze kujikimu kupitia mitambo ya kisasa na aweze kufanya kazi ambayo sisi tunamuagiza kama Bunge Tukufu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, yapo masuala ambayo mimi ninapenda niyaongelee. Kuna suala la ucheleweshwaji wa utungaji wa sheria ndogo. Juzi Mheshimiwa Kemilembe wakati ana-wind up report yake, lakini pia hata leo nafikiri nimemsikia Mheshimiwa Naibu Waziri wa Mazingira, ali-cite Sheria ya Wanyamapori ya mwaka 2009.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi linanisikitisha sana. Sheria ya Wanyamapori ya mwaka 2009 mpaka leo hatuna kanuni ndogo zinazoongelea ushoroba. Ninapoongelea kutokuwepo kwa kanuni ndogo tayari ni mzigo mkubwa kwa Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba nitoe takwimu zifuatazo, kutokuwepo kwa utungaji wa Sheria hii Ndogo ya Masuala ya Ushoroba imeleta madhara yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mwaka mmoja kuanzia mwaka wa jana mwezi wa kwanza mpaka mwaka huu tumekuwa na vifo vya Watanzania 484 kwa nchi ya Tanzania, lakini pia tumekuwa na hasara hekta 42,000 kwa nchi ya Tanzania ambayo inaitaka Wizara ilipe fidia ya shilingi bilioni moja kwa madhaifu haya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi sote ni Wabunge, tukiwa Bungeni hapa tulisikia tembo wamekatisha, anapita anaenda UDOM. Ninajiuliza tunahitaji nini? Je, tembo hawa waingie hapa ndani ndipo tujue madhara yanayotokana na sheria hii? Inasikitisha sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapoongelea ucheleweshaji wa utungaji wa sheria hii, mamlaka inayohusika na masuala mazima mipango miji imeshindwa kuzingatia taratibu na hatimaye hizi corridor za wanyama zimekuwa zikitumika na kubalishwa matumizi, na hata leo hii tunakuwa na majengo makubwa.

Mimi ninaomba serikali tujifunze kwenye ujenzi wa Jengo la TANESCO. Tumejenga kwa billions of money, pesa za Watanzania baada ya siku mbili tunashusha ghorofa.Tujifunze kwenye hili ni lazima tuweze kutunga sheria hizi ili tuweze kuondokana na mizigo isiyo ya lazima kwa serikali yetu ya Jamhuri ya Muungano. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitapenda niongelee suala zima la ushiriki wa wanakamati kwenye masuala ya kuisimamia serikali yetu. Ukisoma Ibara ya 63(2) inasema; “Bunge itakuwa ndicho chombo kikuu cha Jamhuri ya Muungano ambacho kitakuwa na madaraka, kwa niaba ya wananchi, kusimamia na kuishauri Serikali ya Jamhuri ya Muungano na vyombo vyake vyote katika utekelezaji wa majukumu yake kwa mujibu wa Katiba hii.”

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaombe kwa masikitiko makubwa, Kamati yangu ikiwa tulipata safari ndefu tukasafiri kwa muda mrefu nafikiri ilikuwa safari haikuzidi dakika kumi kwa sababu tulikoka jengo la Bunge hapa tukaenda pale Sabasaba nakumbuka…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. ESTER M. MMASI: Mheshimia Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa na ninaomba kuunga mkono hoja.