Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Naomba nichukue nafasi hii kwanza kuipongeza Serikali Baraza la Mawaziri na wataendaji wote Serikalini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nina mambo machache, kama ambavyo waheshimiwa wajumbe wenzangu wamezungumza kuhusu Wakala huyu wa Barabara Vijijini, naomba Serikali katika bajeti inayokuja ije na utaratibu wa kubadilisha hizi sheria za mgao wa fedha kwenye Mfuko wa Barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha hizi za TARURA hazitoshi zilizokuwa zinatolewa. Kama ambavyo tunaona kwenye Wilaya tulizotokana na Halmashauri tulizotoka daraja la korongo moja halitoshi kwa fedha ambayo anapewa TARURA, sasa kwa kuwa maeneo ya vijijini yamekuwa na ongezeko kubwa na vyombo vya usafiri na mahitaji makubwa ya mtandao wa barabara tungeomba basi Wizara yetu na hata Serikali waone umuhimu wa eneo hili la wakala huyu TARURA kuongezewa fedha za mfuko wa barabara zinazomilikuwa na Serikali za Mitaa maeneo ya mijini na vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ni eneo la ahadi za Rais. Mheshimiwa Rais sasa tuna miaka miwili na zaidi tangu uchaguzi mkuu umepita. Alihaidi ahadi nyingi za bara bara katika maeneo mengi ya vijijini. Kwa mfano katika jimbo langu la Mbulu Mjini alihaidi barabara ambayo haipo kwenye mtandao wa TANROADS. Sisi Wilaya tukasubiri TANROADS atakuja kutekeleza hiyo ahadi ya kilometa tano ya lami. Kumbe barabara alizoahidi sasa hivi mmiliki na msimamizi na mtekelezaji ni TARURA. Kwa hiyo, nimuombe Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI akija wakati anatoa mrejesho aone umuhimu wa kuona barabara zile ambazo zimeahidiwa na Mheshimiwa Rais kwenye mtandao wa barabara ambao TARURA atahudumia kwenye bajeti hiituanze utekelezaji wake, kwa maana ya kuzitengea fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ajira, Serikali ilikuwa na nia njema ya kutaka kuajiri pengine nafasi kama 50,000 hivi katika mwaka wetu huu ambao umebaki miezi minne. Basi hata kabla ya mwaka huu kuisha tuone ni namna gani nafasi kadhaa zitaajiriwa ili kupunguza hii gap kubwa ya mahitaji makubwa ya ajira. Tuna nafasi nyingi kwenye Serikali za Mitaa hasa za Watendaji wa Vijiji, Watendaji wa Kata, walinzi na wapishi na watu mbalimbali ambao ni kada mbalimbali katika nafasi za ajira. Kwa hiyo, nafasi hizi zingeajiriwa hata sehemu ili kupunguza ukubwa wa tatizo hili kama ilivyo sasa hivi na hali hii itasaidia ni kwa namna gani walau tunapata watu ambao watakuwa watenda kazi katika Mamlaka za Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la upelekaji wa fedha za mradi ya maendeleo. Nilikuwa namuuliza Mkurugenzi wa kwetu, fedha hadi sasa kiasi kilichopelekwa ni kidogo sana nilikuwa naomba basi fedha za mradi ya maendeleo hata kwa hii robo iliyobaki ipelekwe kwa kiasi kizuri ili kupunguza hali hii ya ukosefu wa fedha za miradi ya maendeleo kwenye ngazi za Halmashauri. Kwa sasa tuna mahitaji ya miradi ambayo tumeahidi kwa wananchi lakini bado hatujapata nafasi ya kupeleka fedha kwa kiasi kizuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa sekta ya miundombinu kwa ajili ya ujenzi holela mijini, katika Kamati yetu tulikuwa tumependekeza Serikali ione umuhimu wa kuandika waraka kwa Serikali za Mitaa kwenye Halmashauri ili na wale Maafisa Mipango Miji na Wakurugenzi wadhibiti ujenzi holelea unaoendelea kwenye maeneo ya miji yetu ili kuepuka gharama kubwa ya uvunjaji wa majengo hapo baadaye. Kwa vyovyote vile nimuombe Mheshimiwa Waziri, nampongeza sana Mheshimiwa Jafo, Wakurugenzi wanapokuja kwenye Kamati yetu safari hii waje na utaratibu wa kiasi gani walitoa fedha za asilimia 10 ya akina mama kwa mwaka huu wa fedha ili tuone ni kwa namna gani jambo hilitunalozungumza muda mrefu limetekelezwa kwa kiasi na linaweza kuwa na dira nzuri katika utekelezaji ule wa kawaida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la mahakama, tumekuwa na mahitai makubwa ya mahakama, tumekuwa na hali ngumu ya wananchi kufuata huduma ya mahakama mbali. Tutafute ni namna gani walau kwenye tarafa tunakuwa na mahakama, kwa hivi sasa zinaemewa zaidi ya kilomita kama 50…(Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)