Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Godbless Jonathan Lema

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arusha Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. GODBLESS J. LEMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na ninaomba niwakumbushe Wabunge wote kwamba hili ni Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wabunge ndio watunzi wa sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Wabunge ndio watunga sera za maendeleo ya taifa hili. Unapokuwa na chombo kama hiki na mizaha ya ajabu ajabu kama inayoendelea, this is the very serious humiliation for this country. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kutoa pole kwa Mheshimiwa Spika, nafahamu yuko India kwa ajili ya check-up na matibabu na vilevile Mheshimiwa Lissu ambaye na yeye yuko Ubelgiji kwa ajili ya matibabu. Mheshimiwa Spika anatumia fedha za Bunge za Serikali kwa ajili ya matibabu na Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Mheshimiwa Lissu tumeendelea kuumkusanyia fedha mitaani kwa vikopo naye vilevile ni Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekti, hii double standard inayoendelea katika taifa hili, kwamba Mbunge wa Chama cha Mapinduzi anaweza akatibiwa na Serikali, akatibiwa na Bunge, Mbunge anayetokana na upinzani, Chief Whip aliyepigwa risasi Dodoma hawezi kutibiwa na Bunge wala hajapelekewa shilingi mia moja na Bunge. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bob Marley ana wimbo unasema only time will tell.

T A A R I F A . . .

MHE. GODBLESS J. LEMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, tunajadili Taarifa ya Utawala Bora Katiba na Sheria. Kuna Chief Whip wa Opposition kapigwa risasi, kifungu namba 24(1) cha Sheria cha uendeshaji wa Bunge kinaeleza ni nani anapaswa kuwa responsible in case Mbunge amepata matatizo, na kama sitaweza kujadili maslahi ya Wabunge si Lissu peke yake ya Wabunge wote akiwa ameumia ama hajaumia, niko tayari nisiwe Mbunge. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama sisi ni Wabunge hatuwezi kujadili maslahi ya Wabunge, huyu anasimama anaongea mzaha…

MWENYEKITI: Ongea na kiti.

MHE. GODBLESS J. LEMA:… kuna mtu amepotea mpaka leo anaitwa Ben Saanane, kuna watu wanapotea, haya ni mambo yanahusu utawala bora, katiba na sheria, na haya mambo ni ya msingi kuliko madaraja kuliko lami. Uhai wa mtu mmoja unazidi kilometa bilioni moja za lami, haya mambo tukiyajadili kwa mioyo ni msingi imara kwa sababu kuna watu wamepotea, kuna mtu ameumia, yuko hospitali tunapojadili hatuwashutumu tunataka mrudi kwenye sense, mjue kwamba tunajadili damu za watu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo sababu nikasema Spika ni Mbunge, anatibiwa na hela ya Serikali, Lissu ni Mbunge anatibiwa na nani hata tunamchangia fedha? Nataka tulirudishe Bunge kwenye sense, kwamba yuko ndugu yetu anaumia, wewe umempiga risasi, si wewe? Kama Bunge tuongee, haya si kuyajadili kwa mioyo, tena tuna hekima kwamba tunaendelea kujadili huku tunalia na tunafanya sala ingekuwa ni nchi nyingine watu wangeweza kuingia barabarani kwa sababu kuna mtu ameumia. Tunajadili mambo haya anaibuka mtu tu kama mrembo huko pepepepe! Wewe! Wewe! Wewe! (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)