Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi mchango wangu ni katika maeneo matatu kwa kifupi kabisa ni kwamba nazipongeza sana Kamati zote kwa jinsi ambavyo wameandaa kazi zao na jinsi walivyowasilisha taarifa zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye upande wa elimu ya msingi na sekondari hii changamoto ambayo imeletwa na elimu msingi bila malipo tunahitaji wote kushirikiana. Tunahitaji kuhamasisha wananchi waendelee kuchangia ujenzi wa madarasa, ujenzi wa nyumba za walimu, mabweni, mabwalo, maktaba pamoja maabara, Serikali peke yake haiwezi kuachiwa jukumu hilo maana mahitaji ni makubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili ni kuhusu agizo la Serikali kuzitaka Halmashauri kutenga …

(Hapa baadhi Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu agizo la Serikali kuzitaka Halmashauri kutenga asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa ajili ya Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake na Vijana, imezungumzwa kwamba hakuna sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukirejea chimbuko la Mfuko wa Vijana ulionzishwa mwaka 1993 ulianzishwa chini ya kifungu cha 17(1) cha Sheria ya Hati ya Idhini ya Malipo na Ukaguzi (Exchequer in Ordinance) Sura ya 439. Kwa hiyo, inatakiwa tu labda kama ni marekebisho tufanye marekebisho badala ya kusema kwamba hakuna kabisa sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho ambalo ningependa kuchangia ni kuhusu maji vijijini. Ninaomba kuwasihi Waheshimiwa Wabunge, pamoja na utekelezaji unaoendelea ambao mzuri kasi zaidi itaongezeka kupitia Wakala wa Maji Vijiji, nadhani mambo hayo matatu yanatosha yawe mchango wangu.