Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Mohamed Omary Mchengerwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rufiji

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA – MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenywekiti, na mimi nianze kwa kumshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha kusimama mbele ya Bunge lako Tukufu kwa mara nyingine.

Pili niwashukuru Wajumbe na Wabunge wote wa Bunge lako la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao wamechangia kwa namna moja ama nyingine kufanikisha taarifa yetu hii ya mwaka.

Mheshimiwa Mwenywekiti, tumepokea wachangiaji saba ambao wamezungumza mbele ya Bunge lako Tukufu, na wachangiaji wawili walituletea michango yao kwa maandishi. Kimsingi michango iliyotolewa na Waheshimiwa Wabunge ni michango ya kawaida ambayo binafsi ninaamini kabisa kwamba wanaunga mkono Taarifa ya Kamati. Nimshukuru sana Profesa Kabudi kwa niaba ya Serikali pamoja na Mheshimiwa Jenista Mhagama na Mheshimiwa Ikupa na wote kimsingi wameunga mkono hoja za Kamati. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie kidogo baadhi ya mambo ambayo yameibuka nayo ni kuhusu watuhumiwa kutofikishwa katika Mhakama ya Mafisadi ambayo imezungumzwa na Mheshimiwa Taska Mbogo lakini pia ukiukwaji wa Ibara ya 13 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kwa askari polisi kukusanya faini kwa kutoza faini na kuwalazimisha wale wanaowakamata kutokana na makosa mbalimbali ya traffic kulipa faini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia makosa mbalimbali ambayo hayajaainishwa kwenye Sheria ya Makosa Barabarani kutozwa faini na polisi wa usalama wa barabarani ambayo inakiuka Ibara ya 107 kama ambavyo Mheshimiwa Amina Mollel ameizungumza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Mheshimiwa Daniel Mutuka amempongeza Mheshimiwa Rais kusaini sheria mbalimbali ambazo zimetungwa na Bunge lako hili tukufu pamoja na Mheshimiwa Jaku ambaye yeye alizungumzia kuhusu kesi za mahabusu kukaa muda mrefu Mahakamani, vilevile pia kwamba inakuaje kosa linatendeka Zanzibar na mshitakiwa unaletwa Tanzania Bara kushtakiwa. Pia amezungumzia kuhusu Mahakama ya Kadhi pamoja na kuhusu kipengele cha mafuta na gesi ili kuridhia Zanzibar nao kuwa na haki katika jambo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mmasi pia amezungumzia kuhusu Ofisi ya CPD, Mheshimiwa Zacharia amezungumzia kuhusu mabadiliko ya Sheria ya Barabara ambayo imezungumzwa na Waheshimiwa Wabunge mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, labda nianzie Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Mahakama ya Mafisadi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni Bunge lako hili Tukufu ambalo lilifanya marekebisho ya Sheria Namba Tatu ya mwaka 2016 na kutunga Sheria ya Mafisadi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa ni jukumu la Mahakama kwa kuwa Mahakama ndiye mwamuzi wa mwisho kabisa katika utoaji haki kamati yangu inaendelea kuikumbusha Serikali kwamba wale wote waliotuhumiwa ni vyema wakafikishwa mbele ya mahakama. Kwa kuwa ni lengo la Serikali na lengo la Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupigania ufisadi pamoja na rushwa basi ni vema wale wote walishitakiwa kwa makosa mbalimbali ambao hawajafikishwa mahakamani waweze kufikishwa mahakamani ili Mahakama itoe tafsiri na kuamua kesi ambazo ziko mbele yao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Susan Lyimo amezungumzia kuhusu mabadiliko ya Sheria ya Ndoa. Labda niseme tu kwamba kwa kuwa kesi hii inayohusiana na masuala haya ipo Mahakamani na Mheshimiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali nakumbuka siku moja, mbili zilizopita amelizungumza jambo hili naomba na mimi kwa kutumia Sheria ya Kinga na Madaraka ya Bunge nisilizungumze kwa sababu nitakuwa nakiuka matakwa ya sheria husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia Mheshimiwa Mary Muro Deo naye alituandikia akizungumzia kuhusu uchelewashaji wa kesi mahakamani. Kwa kuwa taarifa yangu imejieleza kwa kina kuhusu sababau za msingi za ucheleweshaji wa kesi mahakamani ninaomba Serikali ijielekeze katika utekelezaji wa maagizo ambayo Kamati yangu imetoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na kuhusu suala la changamoto za Muungano kuhusu masuala ya mafuta na gesi, jambo hili kwa kuwa liliwahi kujadiliwa kwenye Kamati yangu, nimkumbushe tu Mheshimiwa Jaku kwamba jambo hili tayari lilishashughulikiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Tunatambua kwamba hii ni sehemu ya changamoto kubwa zilizoibuka wakati wa mjadala wa Katiba Mpya, lakini tunatambua kwamba Serikali yetu kupitia Wizara ya Muungano tayari ilishatoa maelekezo kwa Wanasheria Wakuu wa Serikali wote kutoka Tanzania Bara na Tanzania Visiwani kukaa na kutunga sheria kuona utaratibu mzuri wa kuweza kutatua jambo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niipongeze sana Bunge lako tukufu kwani mwaka 2015 tayari imetunga Sheria ya Mafuta na Gesi. Sheria hii imekwenda kufuta sheria iliyokuwepo ya Mafuta na Gesi ya mwaka 1984 sheria ambayo ilikuwa haiitambui Zanzibar katika mchango wa kuchunguza lakini pia kushughulika na masuala ya mafuta na gesi. Kwa hiyo, jambo hili tayari limeshashghulikiwa kwa kutokana na changamoto iliyokuwepo na tayari mchakato huu umeshasha fanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini …….

T A A R I F A . . .

MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA – MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti kwa kuwa jambo ambalo ndugu yangu analizungumza lipo katika Nyongeza ya Kwanza ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ninatambua kwamba mabadiliko ya katiba ndiyo yatakayoweza kuliondoa jambo hilo katika sehemu ya Muungano, lakini kwa hatua iliyopo sasa Serikali tayari imeshalifanyia kazi na ndiyo maana Bunge lako hili tukufu lilitunga Sheria ya Mafuta na Gesi mwaka 2015 na kupitishwa mbele ya Bunge lako tukufu. Pia ninazo taarifa kwamba Zanzibar tayari pia wanayo Sheria ya Mafuta na Gesi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na mchakato wa watuhumiwa kuhamishwa kutoka maeneo mbalimbali kule Zanzibar na kuletwa hapa Bara, nimuombe ndugu yangu ajielekeze katika Ibara ya nne ya Katiba ambayo inaizungumzia jambo hili. Pia sitaki kwenda mbele sana huko kwa kuwa Waziri wa Katiba na Sheria atayatolea ufafanuzi masuala haya iwapo utayaleta mbele yake, niombe tu kuhitimisha hoja yangu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kueleza kwa kina shughuli zilizotekelezwa na Kamati, maoni na mapendekezo ya Kamati naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako sasa liipokee na kuikubali Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kama Maazimio ya Bunge hili. Naomba kutoa hoja.