Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Bernadeta Kasabago Mushashu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. BENARDETHA K. MUSHASHU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami niweze kuchangia kwenye hoja hii. Kwanza kabisa nampongeza Mheshimiwa Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii pamoja na Kamati nzima na Kamati ya UKIMWI kwa kazi nzuri waliyofanya ya kuchambua taarifa za utekelezaji wa Wizara mbalimbali na kuweza kuyaleta mapendekezo mbalimbali. Nasema hongera sana, nami naunga mkono hoja mapendekezo yaliyoletwa mbele ya Bunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naanza na afya, napenda kuchukua fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri kwa utendaji mzuri sana, wamefanya mambo makubwa sana kwenye upande wa afya. Wote tumeshuhudia operations kubwa sana zinazofanywa kwenye Hospitali ya Mifupa ya MOI, wote tumeshuhudia operation za kileo zinazofanyika kwenye Hospitali ya Moyo ya Jakaya Kikwete, wote tumeshuhudia hata upandikizaji wa figo sasa hivi unaweza kufanyika Tanzania na watu wanatoka nchi za jirani kuja Tanzania kupatiwa huduma hizo. Kwa hiyo, nasema hongera sana kwa kazi nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na ugonjwa wa cancer. Ugonjwa wa cancer ni ugonjwa wa ambao umesambaa sana, sasa hivi watu wengi wanaugua ugonjwa wa huu. Kuna cancer ya damu, ubongo, tezi dume, mlango wa kizazi, cancer matiti; kwa hiyo, cancer ziko za aina nyingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili mtu aweze kugundulika kabisa ana cancer, iwe confirmed, anapaswa afanyiwe vipimo vingi ikiwemo na CT-Scan. Unakuta gharama ya vipimo hivyo hasa kwenye Hospitali ya Bugando ambayo kwa Mkoa wa Kagera tunatumia hiyo, unakuta vipimo vina- cost kati ya shilingi 500,000 mpaka shilingi 600,000 kuweza kugundua kama huyu ana cancer kweli au hapana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda sasa kwenye matibabu labda amewekewa chemo, dose moja ni kati ya shilingi 600,000 mpaka shilingi 700,000. Je, hawa Watanzania tunaowajua na uwezo wao mdogo waliokuwa nao, ni wangapi wanaweza ku-afford kulipa hizo hela zote kusudi wagonjwa wao waweze kupata matibabu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, napendekeza kwa Serikali yangu sikivu na Mheshimiwa Waziri kwamba kwa ugonjwa huu wa cancer na kwa wingi na ukubwa wa tatizo lilivyojitokeza, Serikali ingeweka ruzuku kwenye dawa za ugonjwa wa cancer kusudi dawa hizi ziendelee kutolewa bure katika hospitali zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuwa Wizara imefanya kazi nzuri sana kwenye Hospitali za Rufaa kama Muhimbili na nyingine zote, nilikuwa naomba sasa concentration iende kwenye Hospitali za Mikoa, Hospitali za Wilaya, Vituo vya Afya pamoja na Zahanati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kuzungumzia Mkoa wa Kagera; ukienda mkoa wa Kagera utakuta karibu Wilaya zote hazina Hospitali za Wilaya, sana sana tunadandia kwenye hospitali zile za mission.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na Wilaya ya Kyerwa. Wote tunajua kwamba Wilaya Kyerwa ni mpya, hawana kabisa Hospitali ya Wilaya, wanatumia pale Isingiro pamoja na Nkwenda ambapo sana sana zile ni sawasawa na zahanati. Nilikuwa naomba Serikali iwasaidie kwa kuwa ni Wilaya mpya hii, iweze kupata Hospitali ya Wilaya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda pale Manispaa ya Bukoba, tangu mwaka 2013 wanajenga Hospitali ya Wilaya. Wameshindwa kwa sababu huu ni mradi mkubwa, kwa bajeti za Halmashauri hawawezi kuukamilisha. Nilikuwa naomba Serikali isaidie kukamilisha Hospitali ya Wilaya ya Manispaa ya Bukoba ikiwemo vilevile na Hospitali ya Wilaya ya Muleba. Hospitali ya Wilaya ya Muleba wananchi walijitahidi, wamejenga majengo mazuri, ila haijakamilika. Sasa hivi MSD wanapatumia pale, wakiondoka yataendelea kuwa magofu na zile juhudi za wananchi zitaharibika bure.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali itusaidie, kwa kuwa hii ni miradi mikubwa na najua siyo kwa Kagera peke yake, kuna maeneo mengine waendelee kutusaidia kuweza kukamilisha hii miradi kusudi huduma ziweze kutolewa kama ilivyokusudiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wote tunajua kwamba katika Mkoa wa Kagera tulipata tetemeko la ardhi. Tulipata athari nyingi, watu walifariki, taasisi mbalimbali ziliathiriwa na nyumba za watu zimeanguka na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kuzungumzia Kituo cha Afya ambacho kiko katika Wilaya ya Misenyi kinaitwa Kabyaile. Hiki kituo kimejengwa kwa nguvu ya Kamati ya Maafa ambayo ni michango ya wananchi na ya Serikali, ni kituo kizuri sana kimejengwa, hata Rais alishapelekwa kukikagua kile kituo. Pamoja na majengo mazuri, kuna theatre lakini hakuna vifaa, kuna mortuary lakini hakuna mafriji na kuna laundry lakini hakuna vifaa vya kusafishia. Naomba Serikali itusaidie kuweka hivyo vifaa kusudi Kituo cha Afya cha Kabyaile kilicho Ishozi, Misenyi kiweze kuanza kufanya kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie Hospitali ya Mkoa wa Kagera ambayo inaitwa Bukoba Government Regional Referral Hospital. Hii ndiyo kimbilio la mkoa mzima. Wilaya zote tunategemea hii hospitali, lakini haina wataalamu, ina Madaktari Bingwa wanne tu ambao ni wa meno, wa watoto pamoja na wa macho. Wanne kati ya Madaktari Bingwa kama 24 wanaotakiwa. Ukienda kwa wauguzi, hao ndio kabisa. Kwa hiyo, tulikuwa tunaomba Serikali kwa hospitali hii ipatiwe wataalamu kusudi iweze kufanya kazi. Hatuna surgeon, hatuna daktari wa mifupa. Wote mnajua accidents za boda boda ni kila siku. Sasa bila kuwa na hawa Madaktari Bingwa inakuwa ni shida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hiyo hospitali, kuna wodi ya wazazi ambayo ni ndogo sana. Ina vitanda sita tu na hii ni Referral Hospital ya Mkoa, havitoshi na hakuna theatre. Mwanamke akitoka kule, ana uchungu, akaletwa pale kwenye Regional Hospital, akakuta ile multpurpose theatre ambayo na yenyewe ni ndogo, kuna mtu anafanyiwa operation, inabidi huyu mama amcheleweshe. Kwa hiyo, inabidi huyu mama afe kwa sababu amekuta ile theatre inatumika. Tulikuwa tunaomba basi, katika Hospitali ya Mkoa ijengwe labour ward kubwa ikiwa na theatre yake ili tuweze kupunguza vifo vya mama na mtoto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile tukumbuke kwamba Mkoa wa Kagera hatuna mahali pa kukimbilia; ukienda huku ni Uganda, ukienda huku ni Rwanda; ukienda huku ni Burundi; sana sana umkimbize mgonjwa kumpeleka Bugando ambayo iko something like kilometa 500 kutoka Mkoa wa Kagera. Ukitaka kutembea kwa meli ni masaa kama manane mpaka 10 au ukizunguka lile ziwa. Tulikuwa tunaomba ile hospitali ipewe ambulance, kwanza na Mheshimiwa Waziri Mkuu alishakuja akaahidi pale kwamba atatoa ambulance. Namuomba Mheshimiwa Waziri Ummy, hilo alichukue kwamba Hospitali ya Government Regional Hospital waweze kupata ambulance kwa sababu ni mbali sana na Bugando waweze kufanya hizo kazi zinazotakiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawapongeza sana Wizara ya Elimu kwa kazi nzuri mnayofanya. Nawapongeza kwa uamuzi wenu wa kuweza kukarabati zile shule kongwe. Wote hapa tumesoma zile shule za zamani, shule kongwe karibu
100. Pia naomba Mheshimiwa Waziri aikumbuke na shule yangu, mimi nilikuwa Mkuu wa Shule pale, lakini ni shule ambayo inasomesha wanafunzi wengi wasichana, Shule ya Rugambwa Sekondari na yenyewe imeanza tangu mwaka 1965 inahitaji ukarabati mkubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kuzungumza juu ya matamko ya Waziri wa Elimu. Mheshimiwa Waziri hivi juzi ametamka kwamba watoto ambao watashindwa kufikia ile alama ya ushindi au pass mark wasikariri madarasa. Sasa hapa mimi nazungumza kama mwalimu. Huyu mwanafunzi asipokariri darasa au huyu mtoto aliyeshindwa kufikia alama ya ufaulu, kwa mfano akapata sifuri kati 100, akapata 10 kati 100, akapata 20 kati ya 100 tunamwambia apande tu darasa, tunakuwa tunamsaidia huyu mtoto au tunamlemaza?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukumbuke kwamba watoto wengine hawataki kusoma. Tukumbuke kuna mahali ambapo walimu hawataki kufanya kazi. Sasa kwa nini huyu mtoto badala ya kumpitisha tu akafika form four akapata division zero, akikariri anakuwaje? Mbona hata humu ndani kuna wengi walikariri na wala hawakuathirika? Napendekeza kwamba watoto wawe wa private au wa government, yeyote ambaye atashindwa kufikia alama ya ufaulu akariri darasa tusije tena tukaanza kukimbizana kuangalia namna ya kufuta zero. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie kuhusu shule za private. Kabla mzazi hajampeleka mtoto private anatafuta mwisho anapata shule moja, anaangalia ile shule ina vigezo gani? Wanataka nini? Discipline ikoje? Ufaulu ukoje? Karo ikoje? Mzazi mwenyewe anachagua kwamba anataka kumpeleka kwenye shule fulani ambapo wengine wanatoza karo kubwa, lakini mzazi anaamua anamtafutia mtoto elimu bora, anampeleka kwenye ile shule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa naomba Serikali kama inawezekana, hizi shule za private wangeziacha na alama zao za ufaulu kwa kuwa wazazi hawalazimishwi na wala wanafunzi hawalazimishwi kwenda kwenye hizo shule. Wazazi wanawapeleka kabisa kwa mapenzi yao, wawaache kusudi waweze kuwapeleka kwenye hizo shule na pass mark iendelee kuwa zile zile kama shule watakazokwenda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema hivyo kwa sababu leo tunajivunia, naona Wizara tunatangaza kwamba baada ya mtihani wa form four, kati ya shule kumi za kwanza au bora zilizofanya vizuri unakuta most of them ni za private ambao walikuwa wameweka viwango vya ufaulu. Kwa hiyo, nilikuwa naomba nishauri kama Mwalimu kwamba shule za private waziache ziweze kuweka ufaulu wao na hii itasaidaia kuboresha elimu katika nchi yetu ya Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho kabisa naunga mkono hoja.