Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE.RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na juhudi ambazo Serikali inafanya kuhakikisha inapunguza magonjwa yanayoambatana na Ugonjwa wa UKIMWI kama TB na Magonjwa ya Zinaa, pamoja na majukwaa maalum ya Elimu zinazofanyika, bado maambukizi katika jamii yapo hususani katika eneo la vijana linaloambatana na matumizi ya madawa ya kulevya, je Serikali, haioni iko haja ya kuhakikisha vijana wanapata ajira ili kupunguza tatizo hili la chakula/lishe na UKIMWI.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkakati wa Serikali katika eneo hili pamoja na kuhakikisha jamii inapata aina ya vyakula vinakua na lishe, hivyo iko haja ya Serikali kuhakikisha mfumo wa viwanda hivi tunavyovijenga sasa pia vizingatie suala la kutengeneza nafaka zenye lishe bora na pia kuna wagonjwa Watanzania maskini wanatumia dawa hizi wanashindwa kupata vyakula vyenye lishe bora ili kuwasaidia kupata afya wanapokua wanatumia dawa hizi za kupunguza makali ya UKIMWI. Je, Serikali haioni haja ya kuhakikisha inawapatia vyakula vyenye lishe bora waathirika hawa maskini pindi wanapofika katika dirisha la dawa?

Mheshimiwa Naibu Spika, Ukatili na Unyanyasaji wa Jinsia kwa Waathirika; kwa kuzingatia maoni ya Kamati, naomba Serikali iweke mkazo mkubwa kupitia madawati haya ya unyanyasaji wa kijinsia kutatua kero hii, kesi hizi zimekuwa zikichukua muda mrefu na hivyo kupelekea vitendo hivi kuendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la ajira limekua kiini kikubwa cha tatizo la baadhi ya mikoa kuendelea kusambaa kwa magonjwa haya hususani Mikoa ya Dar es Salaam, Arusha, Mwanza na Morogoro, mikoa ambayo kuna wimbi kubwa la starehe na biashara ya Madawa ya Kulevya imeshamiri na pia wanawake wanaofanya biashara ya kuuza miili yao inaendelea. Hii yote inatokana na ukosefu wa ajira zisizoeleweka. Je, Serikali haioni kwamba ukosefu huu wa Ajira unapelekea maambukizi ya UKIMWI na matumizi ya Madawa ya Kulevya kuongezeka.

Mheshimiwa Naibu Spika, upatikanaji wa dawa za kupunguza makali ya VVU; baadhi ya maeneo vijijini bado ni changamoto hususani waathirika wanaotoka vijijini na hii hupelekea mgonjwa kushindwa kufika hospitali kufuata dawa na hivyo Serikali ione haja ya kuongeza madirisha ya ugawaji dawa. Serikali kusimamia Halmashauri kupitia fedha zinazotengwa kwa ajili ya UKIMWI.

Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo mengi Halmashauri hazitumii pesa hizi kwa mlengwa kuisaidia jamii hii, hivyo Serikali ione haja ya kusimamia katika Halmashauri hizi ili pesa zifike kwa walengwa, kupitia elimu kuhusu masuala ya UKIMWI, Warsha, makongamano na misaada kwa walengwa isiishie tu kulipanalipana posho huku wahusika haziwafikii.

Mheshimiwa Naibu Spika, hali ya Magereza/ Mahabusu, mfano wa Gereza la Kalila, Nkulunkulu na Mahabusu zilizopo katika Manispaa ya Mpanda hali ni mbaya. Hii sio Mkoa wa Katavi pekee bali ni katika Magereza mbali mbali nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, mlundikano wa wafungwa unapelekea utoaji wa huduma za afya bora kushindwa na wanazidiwa uwezo kuna wafungwa na mahabusu 39,312 na uwezo wa magereza ni kuhifadhi mahabusu 29,552. Je, Serikali ina mkakati gani kutatua changamoto hii katika Taifa.