Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Maria Ndilla Kangoye

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. MARIA N. KANGOYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia fursa ya kuchangia hoja iliyopo Mezani. Nianze kwa kuwapongeza Wenyeviti wote wa Kamati zilizowasilisha hoja leo kwa umakini walioonesha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuchangia suala la utoaji wa taulo kwa watoto wa kike lililowasilishwa katika taarifa ya Kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii katika ukurasa wa 41. Ni kweli, ipo haja ya kumkomboa mtoto wa kike kwa kuwagawia taulo safi, ili waweze kukamilisha malengo yao ya kimaisha hususani ya kielimu. Kwa sababu, nchi nyingine za Afrika zimejaribu na kufanikisha, hakika nasi tutaweza. Suala hili ni zito na uzuri Mheshimiwa Waziri wa Afya ni mwanamke na ni imani yangu kuwa atalisimamia vyema kama tunavyotarajia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafahamu ya kuwa hofu kubwa inaweza kuwa katika kuweka uhakika wa watoto hawa kupata taulo hizi kwa wakati, lakini niihakikishie Serikali kwamba, nchi kama Uganda, Kenya, Ethiopia na nyingine ambazo tayari zimethubutu kufanya hivyo, zimefanikisha kwa kugawa taulo za kufua, maarufu kama reusable sanitary pads ambazo ni bora na zinagawiwa mara moja kwa mwaka hivyo, kuepusha gharama kubwa kwa Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, najua mara nyingi taulo hizi zimehusishwa na ukosefu wa maji, ambako kiukweli ni tatizo tofauti kabisa. Tujiulize tunalalamika watoto kukosa taulo salama, je, wanatumia nini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, jibu ni matambala yasiyo salama ambayo pia, yanatumia maji kuwekwa katika hali ya usafi. Hivyo, basi ni muhimu Serikali pia, kuangalia changamoto ya maji kwa afya ya hedhi salama kwa sababu, watoto wa kike na wanawake kwa ujumla ni lazima watumie maji bila kujali wanatumia nini wakiwa hedhini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na naunga mkono hoja.