Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nafasi ya mwanamke na uchumi; kwa kuzingatia maoni ya Kamati mazuri yakifanyiwa kazi katika nyanja mbalimbali nadhani kutamsaidia mwanamke ambaye kimsingi anabeba majukumu makubwa na magumu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekua ikitenga fedha kwa ajili ya mikopo kwa wanawake yenye riba nafuu kupitia Halmashauri na Taasisi za kifedha, je, Serikali haioni kupita mikopo hii kuwa haiwasaidii wanawake maskini na badala yake wanaonufaika ni wale wanaojiweza kiuchumi, Serikali inaondoaje ubaguzi huu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, uhaba wa watumishi wa afya nchini; Mkoa wa Katavi una upungufu mkubwa wa watumishi wa afya, Madaktari Bingwa hakuna, lakini pia Manesi hawatoshi katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda na hii inapelekea kuleta msongamano mkubwa wa wagonjwa katika zahanati na katika madirisha ya dawa na kuna kipindi msongamano mkubwa hupelekea wagonjwa kuzidiwa wakiwa katika foleni wakisubiri huduma na wengine kupoteza maisha wakisubiri huduma kwa madaktari. Je, ni kwa nini Serikali mpaka sasa haijaajiri watu wa kada ya afya?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwa nini Serikali inapata changamoto hizi kila siku lakini, bado hazifanyiwi kazi? Je, Serikali hii haioni na haitaki kufanyia kazi ni kwa nini inaacha walipa kodi wanateseka na huku pesa zinapelekwa katika mambo yasiyo vipaumbele kwa wananchi maskini, mfano, Ujenzi wa Uwanja wa Ndege Chato, E-passport mpya na ununuzi wa ndege ambao kimsingi haujazingatia mchakato wa manunuzi? Ni kwa nini Serikali inazitelekeza huduma za jamii nchini na kujikita zaidi kwa wananchi wasio maskini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukurasa wa 45, Kamati imeshauri Serikali kuja na mkakati wa kudhibiti tatizo la unyanyasaji na ukatili wa kijinsia katika jamii hii wanaoathirika ni watoto na wanawake zaidi na jamii imekuwa ikipeleka taarifa katika Madawati ya Jinsia, Polisi na Mahakama, je, ni kwa nini Serikali inashindwa kusimamia kesi hizi na malalamiko kwa jamii kuhusu suala la kesi kuchukua muda mrefu na hivyo jambo hili kuendelea kufanyika kwa sababu watuhumiwa wanaendelea kutoka wanaposhutumiwa? Je, Serikali haioni kuendelea kukaa kimya na hizi kesi inajenga mazingira ya watuhumiwa kuishi kwa hofu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali ya Afya ya Akili, Mirembe Dodoma; hospitali hii ina changamoto ya nafasi na huku inachukua wagonjwa 317 Wodini kila siku na inahudumia wagonjwa wa akili 43 kwa siku na kuhudumia wagonjwa 119. Kwa uwiano huu hospitali hii ambayo ndiyo kubwa nchini bado hospitali hii haitoshi na majengo yake ni chakavu pamoja na upungufu wa watumishi wa afya. Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha inaboresha huduma katika hospitali hii katika Mji wa Dodoma?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ongezeko la wagonjwa wa akili bado lipo katika Mkoa wa Katavi na kwa kuwa Serikali haifanyi utafiti katika mikoa kuona ni kwa nini ongezeko hili linatokea na nini kifanyike kusaidia jamii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Shule ya Msingi Kashato, Shule ya Msingi Nyerere na Shule ya Azimio, Jimbo la Mpanda Mjini ina watoto wenye matatizo ya akili wengi tu, lakini wana tatizo la kupata madarasa, huduma za vyakula pamoja na Walimu.