Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa fursa, kwanza naunga mkono hoja za Kamati mbili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, shule binafsi kukaririsha watoto; ni ukweli dhahiri kabisa wamiliki wa shule binafsi wa mtindo wa kufanya udahili wa watoto wanaojiunga na pia katika mitihani yao wameweka kiwango cha ufaulu na wastani ni 75/100. Suala hili sio haki kwa watoto ambao huenda mazingira au uwezo wake wasiweze kufikia ufaulu huo, hivyo watoto wanakaririshwa darasa na umri wao unazidi kwenda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo basi, suala la Serikali kutoa mwongozo shule binafsi kutokaririsha watoto naunga mkono kwani hakuna mzazi asiyependa mtoto wake kufaulu. Kwa hiyo, Serikali iendelee na msimamo huo ili haki ya kikatiba itendeke kwa watoto wenye uwezo mdogo. Serikali imeweka mtihani maalum ya kupima watoto kitaifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, madeni yaliyorithiwa toka Wizara ya Afya yameenda Elimu; kuna baadhi ya vyuo vya mafunzo kwa jamii vimehamishiwa Wizara ya Elimu ambapo awali ilikuwa chini ya Wizara ya Afya, mfano Chuo cha Msaginya, Katavi; kuna kazi za ukarabati, mkandarasi hajamaliza miaka miwili imepita wala Serikali haijamlipa. Hivyo, Serikali iangalie madeni pia fedha za uendeshaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, upimaji UKIMWI; Sheria ya UKIMWI inamtaka mama mjamzito kupima kwa lazima ambapo imetekelezwa kwa kiasi kikubwa lakini kwa wenza wa mama wajawazito sheria bado haijawataka wao kwa lazima kupima VVU. Hivyo kuna hoja sheria iboreshwe ili wenza wao nao wapimwe kwa lazima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kikundi cha jamii kingine ambacho ni muhimu sana sheria iwatambue kupima kwa lazima, Serikali iangalie wanafunzi wanaotaraji kujiunga na Elimu ya Vyuo Vikuu ili kulinda maambukizi mapya.