Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie katika hoja kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, upungufu wa Walimu; tatizo la upungufu wa Walimu hasa katika shule za msingi ni kubwa sana. Njombe Mjini inakosa Walimu 454. Nchi hii inaenda kuua elimu kwa sababu hatuwezi kuwa na elimu bora kama hatuna Walimu wa kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia walimu hawa walipandishwa madaraja wakawekewa pesa za kupandishwa madaraja haya, lakini baada ya mwezi mmoja wakasitishiwa pesa hizo. Naiomba Serikali ipeleke Walimu wa kutosha mashuleni lakini pia Walimu wapandishwe madaraja yao na wapandishiwe pesa zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, matokeo mabaya ya mitihani; matokeo ya mitihani ni mabaya sana hasa shule za Serikali. Shule zinazoongoza kuanzia ya kwanza hadi ya 10 ni shule za binafsi. Hata hivyo, shule za binafsi zinakandamizwa sana kana kwamba siyo Watanzania. Naomba Serikali itambue kuwa shule binafsi zinalipatia sifa na heshima Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali itende haki kwa shule za private na za Serikali kwa sababu uendeshaji wa shule binafsi ni mgumu sana, kwa kweli ni huduma tu. Mbaya zaidi kwa wale wanaohudumia watoto yatima na wanaoishi mazingira hatarishi lakini wanasoma katika shule hizo, lakini Serikali inawatoza michango mingi kama ya ukaguzi Sh.5,000 kila mtoto, Sh.15,000 ya Mitihani ya Taifa na Sh.1,000 kila mtoto kwa ajili ya michezo. Naiomba Serikali ione ni namna gani inawasaidia hasa shule za watoto yatima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mikopo ya elimu ya juu ni kitendawili; vijana wengi wenye vigezo vya kupata mikopo wanaachwa. Naiomba Serikali kufanya tafiti kwa umakini namna ya kuwatambua vijana hao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, afya; naomba watumishi wa afya waajiriwe wa kutosha na hasa kwenye vituo vya afya. Pia majengo ambayo yamejengwa na wananchi kama Vituo vya Afya na Zahanati, basi Serikali isaidie kumalizia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.