Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Lucy Fidelis Owenya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. LUCY F. OWENYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kupata nafasi ya kuchangia mfumo wa utoajia huduma wa afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti kuna haja ya kuimarisha mfumo wa rufaa kuanzia ngazi ya chini kutoka zahanati mpaka ufike hospitali aidha ya mkoa au za kanda. Unakuta wagomjwa wengi wanakimbilia kwenda hospitali za ngazi ya juu sababu zahanati hazina wauguzi wala madaktari, hakuna vitanda vya kupima wagonjwa, hakuna dawa na kadhalika. Wafanyakazi wengi kwenye zahanati ni ward attendant.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuweza kuleta ufanisi kwenye zahanati ni vizuri Serikali ukaangalia upya kule tulikotoka na kurudisha zile shule za kufundishia nurses, assistant clinical officers, midwife, rural medical aid na hawa walikuwa specifically trained kufanya kazi katika ngazi za chini, lakini sasa hawapo. Wangekuwepo na vifaa vikawepo kwa kiasi kikubwa tungepunguza sana vifo vya mama na mtoto ukizingatia wananchi zaidi ya 80% wapo vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Serikali 80% ya bajeti yake ingeielekeza kuimarisha hizi zahanati, watu wengi wangeishia kutibiwa kule na kwa kiasi kikubwa tungepunguza msongamano kwenye Hospitali za Rufaa ambako kwa sasa hivi hata mtu akitaka kutumbuliwa jipu unakuta wanaenda hata Hospitali za Mkoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni vizuri pia kuangalia hii sekta ya kada ya dawa za usingizi. Hawa wapo pungufu sana, kuna haja ya Serikali kuwezesha wengi zaidi waweze kufika mpaka ngazi za chini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu nguo za wagonjwa, limekuwa ni jambo la kawaida katika Hospitali za Serikali wagonjwa kutoka na nguo zao majumbani na kulala nazo hospitalini. Hii ni hatari sana kuambukizana magonjwa ya ngozi hata kuleta wadudu kama chawa na kunguni wodini, kila mgonjwa anaotoka mazingira tofauti, ni wakati muafaka sasa kwa Serikali kutenga bajeti kwa ajili ya kununua nguo za wagonjwa wanaolazwa wodini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii huenda sambamba na kuimarisha kitengo cha mapokezi cha emergency. Watu wengi hufia casualty sababu unakuta kitengo hiki sehemu nyingine hazina sehemu ya observation, za kumpumzisha mgonjwa ili ajulikane je, atalazwa au ni mgonjwa wa kupeleka wodini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wagonjwa wengi wenye kuishi na VVU wanapopata magonjwa nyemelezi kama nimonia na kadhalika wanabidi wagonjwa hawa wajinunulie antibiotics wakati wengine hawana uwezo kabisa tu kujua kwamba ni rahisi wao kushambuliwa na magonjwa sababu immune yao ilikuwa imeshuka za ARU ni kwa hii wanapopata magonjwa mengi kupitia kitengo chao cha CTC wasipewe dawa hizo bure?

Mwisho, kwa kuwa kumekuwepo na ongezeko kubwa la magonjwa yasiyoambukiza (NCD) na magonjwa haya yanakumba rika zote ni bora elimu itolewe sasa mashuleni kwa nguvu zote. Wizara ya Afya na Wizara ya Elimu waimarishe elimu ya afya mashuleni.