Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nipongeze na kuunga mkono hoja ya Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niishauri Serikali kuhusu wazee wa Tanzania walio wengi wako katika hali mbaya sana. Hawana chakula, hawana dawa na hawana kadi za bima, Serikali iliangalie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe mikopo ya wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu Serikali iangalie kwani inatolewa kwa upendeleo, wale wenye haki ya kupewa hawapewi na kupewa wasiostahili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, si kweli kwamba hospitali zina dawa za kutosha kwani ni mara nyingi nimefika Hospitali ya Tumbi kupeleka wagonjwa hakuna hata panadol; niiulize Serikali ni vipi dawa ziwepo na mgonjwa aambiwe hakuna?

Mheshimia Mwenyekiti, nipende kushauri kuhusu TFDA, tozo za TFDA ni kubwa mno tena kutozwa kwa dola tena hata kwa product ambazo ni ndogo. Hii imesababisha wajasiriamali kupata shida sana wanapokwenda kusajili product zao. Mfano beer 1H (200C) $ 10 kwa nini kwa dola na si kwa Tanzanian shillings?

Mheshimiwa Mwenyekiti, shule nyingi hazina vyoo na madarasa ya kutosha. Walimu hawatoshelezi wakati mitaani walimu wamejaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe Serikali kuboresha Hospitali ya Milembe iongezewe mgao wa fedha na kuboreshwa.