Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (WALEMAVU): Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Awali ya yote niseme nitajikita zaidi upande wa UKIMWI na niseme kwamba UKIMWI bado upo kwa hiyo, ni jukumu la kila mtu binafsi kujikinga na maambukizi mapya ya UKIMWI kwa kubadili tabia, lakini pia kuendelea kujilinda na zile njia nyingine ambazo zinasababisha maambukizi ya UKIMWI. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hoja za Kamati, Kamati imeshauri kwamba hii sera ya Taifa ya udhibiti wa maambukizi ya UKIMWI imepitwa na wakati. Niseme kwamba mchakato wa mapitio ya sera hii ulianza kufanyika toka mwaka 2010. Baada ya mapitio haya, iligundulika kwamba kuna upungufu na upungufu huu uliwasilishwa kwenye Secretariat Cabinet ambapo katika ile Secretariat Cabinet ilishauri kwamba ufanyike uthamini mpya wa utekelezaji wa sera hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa hivi kinachofanyika ni kwamba TACAIDS wanaendelea kutafuta fedha kutoka vyanzo mbalimbali ili kuona kwamba sasa lile agizo ambalo lilitolewa la upitiaji upya wa hii sera unafanyika. Kwa kipindi hiki cha mpito, Serikali imeendelea kutekeleza vile vipengele ama ule upungufu ambao ulionekana katika mapitio ya hii sera.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia niongelee suala la ushauri ambao umetolewa na Kamati kwa habari ya vile vyanzo vya Mfuko wa udhamini wa Mfuko wa UKIMWI. Kamati imependekeza kwamba kama ilivyo kwenye Road Fund, basi huu Mfuko kuwe kuna tozo ambayo itakuwa inasaidia kutunisha huu mfuko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imepokea ushauri huo na tayari utekelezaji umeshaanza kufanyika na naamini kwamba mapendekezo yatakapoletwa kwenye Bunge lako Tukufu basi Waheshimiwa Wabunge wataunga mkono utekelezaji wa hayo mapendekezo ambayo yatakuwa yameletwa kwa habari ya zile tozo ambazo zitakuwa zimependekezwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo, Serikali pia imeendelea kutenga fedha kwa ajili ya kuhakikisha udhibiti wa masuala ya UKIMWI. Fedha hizi mpaka kufika mwaka jana Desemba, 2017, kiasi cha shilingi bilioni 1.3 zilikuwa zimekwishatolewa kwa ajili ya kuhakikisha masuala ya UKIMWI yanaenda vizuri. Fedha hizi zimekuwa zikitolewa kupitia Wizara ya Afya ambapo mwaka jana ilitolewa milioni 660 ambayo ilitumika kununulia dawa za septrine kwa ajili ya waathirika wa UKIMWI.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala zima la data za maambukizi katika nchi yetu ya Tanzania imekuwa ni changamoto. Kuna Mbunge ambaye alichangia mchana akasema kwamba hizi data ni za miaka mingi. Niseme kwamba hizi data sio za miaka kumi iliyopita kama ambavyo Mbunge amesema, hizi data ni za mwaka jana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye maadhimisho ya Siku ya UKIMWI duniani mwaka jana tarehe 1 Desemba hizi ndio data ambazo zilitolewa na hiyo ni sambamba na hoja ya Mheshimiwa Mjumbe wa Kamati, Mheshimiwa Masoud kwamba Dodoma sio kweli kama ambavyo iko. Hizi ni data ambazo zimetolewa mwaka jana tu Desemba na Dodoma ina maambukizi ya 5.0, sasa hizo za kwako sijui ni za lini lakini kutokana na hizi data za mwaka jana Dodoma inaonesha kwamba kiasi cha maambukizi ni 5.0.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kulikuwa na Mjumbe alichangia kuhusiana na Njombe kwamba Njombe wanaonewa, hizi ni data halisi na Njombe inasemekana kwamba maambukizi ni kiasi cha asilimia 11.4.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa mzungumzaji)