Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nianze kwa kumpongeza sana Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii, Mheshimiwa Peter Serukamba na Makamu wake Mheshimiwa Mussa Zungu na Wajumbe wote kwa kweli kwa taarifa nzuri iliyokwenda shule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nigusie machache tu kwa ufafanuzi. Suala la kwanza Kamati inasema sheria ya Baraza la Michezo na BMT ina upungufu mwingi kwa kweli unaokwamisha utendaji wa baraza. Nakubaliana kabisa na Kamati kwa kweli sheria ni ya siku nyingi sana ya mwaka 1967 miaka 51 iliyopita, najua ilishafanyiwa marekebisho mwaka 71 lakini bado ni miaka 47 iliyopita na tumeshaanza hiyo kazi nzuri ya kuifanyia marekebisho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitumie nafasi hii kumshukuru sana Mheshimiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali na timu yake ya wataalam kwa kukaa na wataalam wangu wa Wizara kuifanyia first drafting hii ya hii sheria na mtaiona baada ya muda si mrefu mbele yenu hapa Waheshimiwa wa Bunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala la uboreshaji wa TBC limeongelewa na Kamati na vilevile Mheshimiwa Amina Moleli naye ameingolea na amezungumzia kuhusu vifaa kwamba vimechoka yeye anaongelea studio mle ndani sawa. Hata hivyo, nataka tu kusema kwamba Serikali inalijua hilo na tumeanza kulifanyia kazi vizuri kabisa sisi hatujaanza kwa mwonekano wa ndani kwa sababu unaweza ukawa na makochi mazuri, lakini kwa kweli huko chumbani kuna matatizo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, sisi tumeanza na mitambo kuboresha usikivu na vile mwonekano wa TBC. Leo hii najua wote nyie mtakuwa mashahidi wangu kwamba mwonekano wa TBC wa picha umeongezeka tena kitaalam wanasema umeongezeka toka asilimia 52 hadi asilimia 88 na yote ni kwa ajili ya ukarabati wa mitambo ambayo inasaidia urushaji wa matangazo. Hata radio za TBC FM na TBC Taifa nazo usikivu wake umeongezeka toka asilimia 60 mpaka asilimia 90 na hiyo yote ni kwa ajili ya ukarabati tunaoufanya wa mitambo yake.

Ukifika pale Mikocheni kuna dude kubwa pale tunaita Satellite uplink ilikuwa wakati huo miaka miwili iliyopita ilikuwa na njia moja tu ambayo tulikuwa tunashindwa kuikarabati, lakini leo zote njia mbili zinafanya kazi na ndiyo maana mwonekano wa TBC umekuwa mzuri zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ipo hoja ya kwamba BASATA iko mbali na wasanii, kwa kweli hapana, si kweli. Nitatoa mifano michache, BASATA huwa inatoa ushauri consultancy kwa wasanii wetu na nitoe mfano mdogo tu wa mwaka jana kuanzia mwezi Julai hadi mwezi Desemba, wasanii 995 wamefika BASATA kupewa ushauri kuhusu kazi yao ya sanaa. Sasa kama hauna mawasiliano mazuri watu 995 katika miezi minne mitano wakafika isingetokea kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tu tukumbuke kwamba pia vijana wetu wengi siku hizi wanaalikwa nje ya nchi kwa ajili ya muziki na ni BASATA inayohangaika kuwapeleka Balozini kuwatambulisha wapate VISA. Kwa kweli mnyonge mnyongeeni, haki yake tumpe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, uboreshaji wa tasnia ya filamu, nakubaliana kabisa na maoni ya Kamati lakini nataka kwamba kama tasinia kwenye sanaa imepiga hatua kubwa sana katika kipindi kifupi ni tasnia ya filamu ambapo leo hii, nadhani sisi ni wa pili kwa Nigeria hata kwa uzalishaji wa filamu kwa mwaka tunazalisha kwa wastani filamu 1,400 kwa mwaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sawa kuna suala la ubora wa filamu zetu kweli zipo zingine hazifurahishi kabisa, lakini katika hizo 1,400 bora zimejitokeza na ndiyo maana leo hii Tanzania tunajivunia tuzo za kimataifa zaidi ya 44 za waigizaji wetu waandaaji wa filamu na kadhalika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile ndiyo maana leo hii hata wawekezaji wamejitokeza sasa kwa ajili ya filamu industry. Leo tunawapongeza sana AZAM TV kwa kuanzisha a dedicated Channel kwa ajili ya sinema zetu za Kiswahili inaitwa Sinema Zetu za Kiswahili. Si hao tu wenzetu multichoice na wameanzisha a dedicated Channel kwa ajili ya sinema za Kiswalihi na sasa hivi tuna TV mpya imeanzishwa Jasson TV ni kwa ajili ya sinema za Kiswahili. Yote haya ni mafanikio yalikuwa hayapo haya ndio yameanza kujitokeza na hii ni ushahidi mkubwa kwamba tasnia ya filamu nchini inaendelea kwa kasi kubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutoka na muda naomba nigusie mambo mawili matatu ambayo Mheshimiwa Devotha Minja ameongelea kuhusu vyombo vya habari. Ameongelea kuhusu maelezo wamemwandikia Tanzania daima barua kwa nini uchaguzi wa Kinondoni wanaandika upande mmoja. Anasema kama wana haki kwa nini hawajawaandikia Uhuru, nimecheka nimemwambia Mheshimiwa Minja ulitaka nao Uhuru wakuletee hiyo barua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, unajua huo ni ushahidi tosha kwamba hata waliokuletea barua hawana weledi, there are not professionals huwezi ukaandikiwa barua na Taasisi ya Serikali na Idara. Badala ya kuwasiliana nao wewe unapeleka kwa Mbunge ni kukosa weledi tu, Uhuru hawawezi kufanya hivyo au gazeti la maana kama Mtanzania na mengine wakakuletea wewe Mbunge hapa barua ambayo ulitakiwa wewe uwajibu, sijui hawajui kujibu wamekuomba wewe uwajibie. (Makofi)

Mheshimwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Minja anasema Waziri nina mamlaka gani chini ya Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 kuweza kuadhibu…

T A A R I F A . . .

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, inanishangaza, namheshimu sana Mheshimiwa Komu, lakini nashangaa leo anaongea utafikiri yeye haelewi, etiquette ya uandishi wa habari kutoka Serikali na kwako basi uwajibie, endelea kuwajibia tu, hongera na utafanikiwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili suala la Waziri kufungia magazeti sio mimi tu, lakini sheria ya mwaka 2016 iko wazi kabisa, akisoma kifungu cha 59 naomba ukaisome, sijui kama umeisoma, kasome vizuri itaelewa. Ni kweli kabisa pengine nitumie dakika chache zilizobaki kwamba tulipotunga hii sheria lengo letu kubwa ni kuanzisha vyombo vya habari ambavyo ni self regulatory ,vinaweza vikajiendesha wenyewe, vikajidhibiti vyenyewe na vitajidhibiti kupitia vyombo vikuu vinne. Hili nimelisema mara nyingi sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vyombo hivi ni:-

(i) Baraza Huru la Wanahabari, Independent Media Council;

(ii) Bodi ya Ithibati;

(iii) Kamati ya malalamiko ambayo tena chini ya sheria hiyo ina madaraka kabisa kama ya Mahakama is a Quasi judicial Body; na

(iv) Mfuko wa sanaa vyombo hivi havijaweza kuundwa kwa sababu ya kipengele ambacho nyie wenyewe Waheshimiwa Wabunge akiwemo la Mheshimiwa Minja kulalamika kwamba hatuwezi kumwadhibu Mwandishi wa Habari moja moja kwa sababu hata weledi bado hawana. Kwa hiyo tuwape kipindi cha miaka mitanowaweze sasa ku- meet requiments za hii sheria za kuwa na Diploma au Degree kuweza kuwa Mwandishi wa Habari kuweza kutambuliwa kwamba hii ni taaluma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tuko katika kipindi hicho cha mpito hatuwezi kufanya chochote. Ningetegemea Mheshimiwa Minja kama una uchungu kabisa wa hii tasinia, hebu njoo tuweze kuondoa hicho kipengele cha transition ili tuweze kuunda hivi vyombo, nitakuelewa vizuri sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.