Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi nami nichangie. Kwanza niwapongeze Wenyeviti wa Kamati zote mbili kwa kazi nzuri wanayofanya, naomba nijikite kwenye ripoti ya Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama.

Mheshimiwa Naibu Spika, Tanzania inatekeleza Diplomasia ya Uchumi kwa sasa na tumeshuhudia Rais Magufuli akitangaza kuongeza nguvu ya vita ya kiuchumi kwa nchi yetu ambayo ni jambo zuri sana, litaisaidia nchi yetu kutoka hapa ilipo, kwa sababu tumeshapata uhuru wa kisiasa ni vizuri tukapata uhuru wa kiuchumi.

Mheshimiwa Naibu Spika, vita hii na Diplomasia hii haiwezi kutekelezwa vizuri kama Taasisi yetu ya Usalama wa Taifa itaendelea kusimamiwa na sheria tuliyonayo inayoisimamia Taasisi hii ya Usalama wa Taifa. Kwa muda mrefu, Taasisi hii imekuwa inashughulika na usalama wa Viongozi zaidi, kuliko kushughulikia usalama wa nchi kwa ujumla na hasa masuala yanayohusu uchumi wa nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ziko scandal mbalimbali ambazo zimekuwa zikitokea katika nchi yetu, ukianzia kwenye EPA, ESCROW, RICHMOND, kwenye Madini na Mikataba mbalimbali mibovu ambayo nchi yetu imekuwa ikiingia. Kwa muda mrefu mambo haya yakitokea tumekuwa tukishuhudia Wanasiasa wakiadhibiwa na Watendaji ndani ya Serikali wengine wakiadhibiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama Taasisi hii ingekuwa inatimiza wajibu wake kwa mlengo wa kulinda uchumi wa nchi yetu, maana yake ingefanya kazi ya kuzuia nchi yetu isiingie kwenye mikataba hiyo mibovu. Kwamba watu wanakwenda wanafanya utaratibu, wanachukua hela za EPA wanagawana, inakwenda kwa muda mrefu unnoticed halafu baadaye tunakuja kuambiwa unajua kuna watu walipiga hela mahali, halafu wanachukuliwa hatua hawa watu wengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, chombo hiki hakinyooshewi kidole, hawaulizwi, hawasemi chochote, nadhani inawezekana sheria tuliyonayo inawafunga mikono kwa namna moja ama nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nilitegemea kwamba Kamati yetu ingeleta mapendekezo, tupitie upya Sheria ya Usalama wa Taifa ili mikono yao iende mbali, wakumbuke jukumu lao la kuhakikisha wanalinda uchumi wa nchi yetu, katika kipindi hichi ambacho tunahama kutoka kwenye Diplomasia ile ya Siasa kwenda kwenye Diplomasia ya Uchumi muda mwingi wautumie huku, badala ya hivi sasa wanavyofanya kubaki tunasikiliza simu za watu, tunafanya mambo ambayo kimsingi nadhani hayalindi uchumi wetu na mwisho wake gharama yake inakuwa kubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nilidhani twende huko, sheria ile iletwe hapa, tuipitie tuone kama yapo mapungufu yanayowafanya tupelekwe huko tunakoenda, mwishowe tutabaki tunalaumiana kila siku, nchi yetu inaingia kwenye mikataba ya hovyo kila siku na wanaoumia na kuathirika wanakuwa ni wale waliopewa dhamana kwa maeneo yale.

Mheshimiwa Naibu Spika, wanaopaswa kushauri tusiingie huko ni akina nani? Maeneo yetu ya bandari, airport na maeneo mengine, nilidhani eneo la kwanza nishauri umefika wakati tupitie upya Sheria ya Usalama wa Taifa...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)