Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Zainab Mndolwa Amir

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. ZAINABU M. AMIRI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuipongeza Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kwa taarifa yake nzuri ya kipindi cha Februari, 2017 hadi Januari, 2018.

Mheshimiwa Naibu Spika, Jeshi la Zimamoto hususan katika Kikosi cha Zimamoto kilichopo Mkoa wa Dar es Salaam kinawalazimisha wafanyabiashara waliopo karibuni Wilaya ya Ilala kununua mitungi ya gesi (Fire extinguish) kwa lazima na kuiweka ndani ya duka la kila mfanyabiashara. Mfanyabiashara asipotekeleza hutozwa faini, badala ya mmiliki wa nyumba kununua mitungi hiyo na kuiweka pembezoni mwa jengo husika.

Mheshimiwa Naibu Spika, najiuliza je, ikiwa moto utatokea usiku na wakati huo mfanyabiashara ameshafunga duka, amelala nyumbani kwake, je mtungi huo uliopo ndani ya duka utamsaidiaje mfanyabiashara kuokoa mali zake? Je, hatuoni kuwa huu ni mradi maalum wa Kikosi cha Zimamoto na siyo kulinda mali za wafanyabiashara?

Mheshimiwa Naibu Spika, maoni yangu wafanyabiashara hao wanaelemewa na milolongo ya kodi nyingi na wakati mwingine kushindwa kuendesha biashara zake na kupelekea kufunga duka. Naomba Wizara husika isaidie kuondoa kero hii na kiuhalisia haina tija yoyote kwa mfanyabiashara ambaye anachangia pato la Taifa kwa kulipa kodi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ufinyu wa fedha hupelekea msongamano wa wafungwa magerezani na pia kuna uchakavu wa majengo ya Balozi za Tanzania. Naomba Serikali itenge fedha za kutosha na kwa wakati ili kupeleka katika Wizara husika kuondoa tatizo hilo. Mwisho nakupongeza Mheshimiwa wa Kamati Mheshimiwa Balozi Adadi Mohamed Rajabu kwa taarifa yako.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.