Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Naibu Spika, kupitia maoni ya Kamati yakizingatiwa na Serikali ikayafanyia kazi, kutokana na changamoto zilizopo kupitia zoezi zima la vitambulisho vya Taifa pamoja na Serikali kutumia pesa kwa ajili ya kutengeneza vitambulisho hivi (NIDA).

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Wizara kuiwezesha NIDA au kuharakisha kuipatia fedha NIDA ili wananchi ambao hawajapata vitambulisho mpaka sasa waondokane na usumbufu huu tukielekea kwenye electronic system kuhusu usajili wa wageni katika mfumo ili kujua kama wanaishi kihalali nchini. Katika zoezi hili Serikali isimamie kwa umakini usajili huu ili kuondoa malalamiko ya wageni kupata vitambulisho vya Taifa na passport kabla ya Watanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika zoezi hili la usajili wa vitambulisho hususan wananchi wa mikoani inaleta usumbufu kusafiri kufuata mikoa yenye huduma hii kama Dar es Salaam na kuwaongezea gharama wananchi. Je, Serikali haioni haja sasa ya kuweka ofisi kila wilaya ili huduma za vitambulisho ifanyike kila wilaya nchini?

Mheshimiwa Naibu Spika, ni jukumu kubwa la Serikali kuangalia masuala yote yanayohusiana na siasa kupitia Jumuiya ya Afrika Mashariki na SADC.

Mheshimiwa Naibu Spika, askari wetu wanajeshi wamekuwa wakichukuliwa kwenda kutuliza ghasia katika nchi zenye vita na ghasia na askari wetu wamekuwa wakipelekwa kutuliza ghasia lakini wakipoteza maisha na kufa Serikali imekuwa ikichukua pesa kuzilipa familia kama rambirambi, lakini baada ya kumaliza msiba mnazitelekeza familia hizo na kuziacha zikiteseka. Je, Serikali ni kwa nini inashindwa kuendelea kuzisaidia familia zao ilihali walikufa vitani huku wakilinda mipaka yetu na kulinda mahusiano ya kidiplomasia? Serikali inalichukuliaje suala hilo ambalo linasababisha askari kuogopa kwenda kulinda amani nje ya Tanzania kwa sababu mnawatelekeza?

Mheshimiwa Naibu Spika, zoezi la usajili wa vitambulisho (NIDA); hivi sasa wapo katika baadhi ya mikoa na zoezi hili linasababisha foleni na msongamano katika ofisi za usajili. Malalamiko ya wananchi ni kutozwa Sh.2,000 katika zoezi hili; je, Serikali haioni kuwatoza wananchi Sh.2,000 na wananchi ni maskini hawawezi kulipia gharama hizi katika mchakato wa kupata vitambulisho? Serikali inawasaidiaje wananchi maskini?

Mheshimiwa Naibu Spika, uwekezaji katika Balozi mbalimbali nchini; pamoja na juhudi za Serikali kupeleka Mabalozi na watumishi katika nchi wakilishi, kuna changamoto, kwa mfano, katika balozi Nchini China (Beijing), kuna watumishi wachache na bado malipo yao yanachelewa, uchakavu wa majengo na asilimia kubwa tumepanga, mfano, Balozi Zimbabwe na watumishi kujibana katika ofisi. Je, Serikali haioni iko haja kuwapatia fedha ili wafanye kazi pamoja na kuweza kutafuta fursa za kiuchumi?