Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchangia katika hoja hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, uchunguzi wa kina kabla ya kutoa adhabu kwa Wabunge; kumekuwa na adhabu mara kwa mara kwa Wabunge na hasa Wabunge wa Upinzani, nimekuwa nikijiuliza ni kwa nini? Nimegundua kuwa Wapinzani wanapoona mambo fulani yanakwenda isivyotegemewa au bila haki kutendeka ndio maana inawafanya kupata hasira na kuropoka au kutenda vitendo kinyume na maadili.

Mheshimiwa Naibu Spika, naiomba kuishauri Serikali kuchunguza ni kwa nini mambo haya yanatokea. Serikali ikitenda haki na usawa na ikiwasikiliza hasa yale wanayoshauri kwa manufaa ya Taifa, watu hawataweza kutenda matendo kinyume na maadili.

Mheshimiwa Naibu Spika, muda wa adhabu; naomba Wabunge waliopata adhabu mwaka jana walipata adhabu ya muda mrefu mno. Naomba adhabu zipunguzwe maana Wabunge wanakosa uwakilishi kwenye majimbo yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, upendeleo; katika kupeleka watu kwenye maadili wanapelekwa wa upande mmoja, ni wale wa kutoka Upinzani tu. Mara nyingi nimesikia maneno ya kuudhi kutoka upande wa Chama Tawala hawachukuliwa hatua yoyote. Naomba kuwasilisha.