Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Naibu Spika, nipongeze taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge.

Mheshimiwa Naibu Spika, nishauri kwamba Uongozi wa Bunge uendelee kutoa elimu na maelekezo juu ya taratibu za Bunge ambazo zitasaidia Wabunge kutambua wajibu wao. Pia nishauri Uongozi wa Bunge kuweka Semina zitakazowaelimisha Wabunge kujua ni yapi mambo ambayo hayatakiwi Mbunge kufanya.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri vilevile uongozi wa Bunge kabla ya Mbunge kupewa adhabu aitwe aonywe na apate muda wa kujieleza ili haki ipate kutendeka.

Hata hivyo, naomba nishauri kuwa Uongozi ujaribu kufuatilia tabia za Waheshimiwa Wabunge ili kutambua tabia zilizojificha kwa Wabunge hao ili wapate kusaidiwa mapema kabla hawajatenda makosa ambayo yanaweza kuathiri utendaji wa kazi zao za Kibunge.

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile nishauri Kamati ya Maadili inaposhughulikia masuala ya Wabunge iweke weledi mbele na iwachukulie wakosaji wote sawa bila kuweka upendeleo wa aina yoyote. Pia nashauri adhabu zinazotolewa ziangaliwe zisiwe zile ambazo zinadhalilisha au kuathiri utendaji wa Wabunge husika kwani wametumwa na wananchi kuwawakilisha hivyo adhabu yoyote ile isiathiri uwakilishi wao.