Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Naibu Spika, kupitia taarifa hii ya Kamati ambayo imetupa picha ya namna sisi kama Wabunge kujua wajibu na haki zetu na mchakato wa kutunga kanuni za maadili ndani ya Bunge. Muda ni finyu sana ambao umekuwa unatengwa tunapotunga sheria hizi na kupelekea Wabunge wasio na taaluma kupitisha kanuni ambazo baadaye huzilalamikia kanuni kuwaumiza hivyo muda uongezwe, hautoshi.

Kupitia kanuni hizi na lengo la Kamati hii katika suala la kutoa adhabu kwa Wabunge, kwa malalamiko ya Waheshimiwa Wabunge ni kwamba Kamati hii iko haja ya kutoa muda kuwasikiliza Waheshimiwa Wabunge kwa undani kabla ya kutoa adhabu ambazo kimsingi ukisoma taarifa ya Kamati inalenga kwa asilimia kubwa kuwapa adhabu Wabunge wa Upinzani kuliko wa CCM.

Je, kupitia Kamati hii na malalamiko ya Wabunge, ni kwa nini kila siku adhabu zinatolewa kwa Wabunge haohao kila siku majina yanajirudia, hamuoni kuwa Kamati ya Maadili badala ya kuhakikisha Wabunge wanapata elimu ya maadili na msikimbilie kutoa adhabu ambayo inapelekea kuleta chuki na sio kufundisha kama lengo. Hivyo, Kamati ya Maadili ione namna ya kuongeza semina kwa Wabunge na Wajumbe wa Kamati pia.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la upendeleo Bungeni, Kamati ione haja ya kuchunguza jambo hili ili likawe Bunge lililotukuka katika ujenzi wa Taifa.