Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, nami nashukuru kwa kupata fursa hii na niwapongeze pia Kamati kwa kazi nzuri waliyofanya. Ninazo hoja mbili tu ambazo nataka kuchangia kutoka kwenye hii Kamati ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama.

Jambo la kwanza, linapatikana kwenye ukurasa wa 21 inalozungumzia suala la alama za mipaka. Suala hili kidogo limekuwa na tatizo na changamoto lakini nilitaarifu Bunge lako kwamba sasa Wizara imepata pesa tumepewa bilioni nne kwa ajili ya kuhakiki mipaka hiyo na kazi zinazokwenda kufanyika ni kukarabati zile pillars zote za zamani ambazo zimechakaa lakini pia na kuweka pillars mpya ambapo hapakuwepo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu pia zilikuwa na umbali mrefu sasa hivi tutakwenda kuweka umbali wa mita 100 kutoka pillar moja mpaka nyingine ili iweze kuonekana na hii inakwenda kufanyika kwenye mpaka wa Tanzania na Uganda pamoja na mpaka wa Tanzania na Kenya kazi hizo zinaenda kufanyika.

Lakini pia kazi nyingine itakayofanyika ni kuwa na ile ramani ya msingi kwa maana ya base map ili kuweza kutambua vilivyoko pale ardhini ikiwa ni pamoja na kusafisha ule Mkuza ulioko pale, kazi hiyo inakwenda kufanyika.

Mheshimiwa Naibu Spika, hapakuwa pia na protocol ya mpaka pale itakwenda kufanyika mwaka huu kwa sababu pesa tulizokuwa tumeweka kwenye bajeti zote zimetolewa na tunaishukuru Serikali kwa kazi hiyo.

Jambo la pili, ni mgogoro wa mipaka ambao umekuwepo katika taasisi nyingi za Jeshi.

Napenda kushukuru sana Wizara ya Ulinzi ambayo iliunda kamati ambayo imepitia katika mipaka mingi inayohusiana kati ya Jeshi na wananchi na wamehakiki mipaka yao yote na maeneo ambayo walikuwa wakiyahitaji wanaendelea nayo na yale ambayo walikuwa hawayatumii na hawayahitaji basi yale watakuwa wameyarejesha baada ya kuwa wameshakamilisha taarifa yao. Lakini kubwa zaidi ni kuzikumbusha taasisi zote...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)