Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dokta John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa hatua anazochukua kukabiliana na Upotevu wa Mapato ya Serikali katika Sekta ya Madini

Hon. Mohamed Omary Mchengerwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rufiji

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dokta John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa hatua anazochukua kukabiliana na Upotevu wa Mapato ya Serikali katika Sekta ya Madini

MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, tarehe 25 Aprili, 2017 nilisimama mbele ya Bunge lako hili Tukufu na nikasema kwamba nchi hii imepata Rais mzalendo namba moja. Niliposimama nililiomba Bunge lako Tukufu kufuta neno uzalendo katika Kamusi ya Kiswahili iwapo siku moja Wabunge walio wengi watasema kwamba mambo yanayofanywa na Dokta Pombe Magufuli siyo uzalendo katika nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, anachokifanya Dokta John Pombe Magufuli ni utekelezaji wa Kanuni ya 10 ya Uongozi (The Law of Connection) ambayo inasema kwamba, leaders touch the heart before they ask for the hand. Mambo haya yaliyofanywa hivi punde ni ya kizalendo na yamemgusa kila Mtanzania katika moyo wake, wale walio katika Vyama vya Upinzani lakini pia hata wale ambao tupo katika Chama Tawala hapa nchini na nje ya nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilichotokea ni uwepo wa mikataba mibovu na nakumbuka wakati nasoma historia nilimsoma Carl Peters mwaka 1884 ambaye aliingia Afrika na kuwasainisha Mababu zetu mikataba ya hovyo kabisa. Leo hii tunajionea uwepo wa mikataba mibovu kabisa hapa nchi ambayo Rais wetu Dokta John Pombe Magufuli amedhamiria sasa kwa kupitia Ilani yetu ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi 2015-2025, ukisoma vyema ukurasa wa 28 na 29 wa Ilani yetu ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi, inazungumzia kuhusu usimamiaji wa madini yetu na kuhakikisha kwamba madini haya yanawanufaisha Watanzania walio wengi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono Azimio letu hili ambalo limetolewa siku ya leo lakini pia niiombe tu Serikali kufuata maelekezo yaliyowahi kutolewa na Keith Jefferis ambaye aliwahi kuwa Deputy Governor kule Botswana ambaye aliwahi kusema kwamba, the paradox of plenty inatokana na kwamba nchi nyingi zenye utajiri wa madini zimekuwa na umaskini wa hali ya juu. Sasa tuombe yale maelekezo yaliyotolewa na Keith Jefferis tuweze kuyafuata katika nchi yetu hii ili sasa madini haya yaweze kuwakomboa Watanzania walio wengi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mambo mengi aliyowahi kuyazungumza Keith Jefferis ni uwepo wa open and transparent katika mineral licensing pamoja na taxation regime. Tuombe uwazi uwepo katika mikataba hii ambayo tayari Rais amekubali kuileta kwenye Bunge hili, uwazi huu utaweza kuisadia nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaamini kabisa sisi Watanzania hususani Jimbo langu la Rufiji wanaamini kabisa kwamba mambo haya yakitekelezwa vyema barabara zetu za kutoa Nyamwage - Utete zitajengwa kwa kiwango cha lami, mambo haya yakitekelezwa vyema basi hata leo hii tusingekuwa na deni la Taifa. Naamini kabisa mambo anayofanya…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)