Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Martha Moses Mlata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikushukuru kwa kunipatia nafasi hii ili niweze kuchangia mjadala huu ulioko mbele yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Dkt. Mpango pamoja na timu yako yote, kwa kweli sisi hatuna mashaka na wewe na kadri miaka inavyozidi kwenda naamini mambo yataendelea kuwa mazuri. So, endelea hivyo na Mungu aendelee kukubariki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesimama hapa nataka nichangie ila kwa huzuni sana, nina uchungu sana, kwa sababu alitokea mtoto mmoja akasoma, akalelewa mikononi mwa wazazi wa Chama cha Mapinduzi, akasoma kwa kodi ya Watanzania na wananchi wa Singinda hususani wananchi wa Ikungi Mashariki, Mheshimiwa Tundu Lissu mdogo wangu. Wananchi wa Singida wakamwamini wananchi wa Ikungi Mashariki, wakampa nafasi nenda baba katutetee, ukatuombee shida zetu huku, wananchi wa Ikungi hivi ninavyoongea wanawake wana taabu, walimwamini kijana wao aje alie ndani ya Bunge ili waweze kupata maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, walimtegemea kijana wao akawakomboe na shida zao. Naomba niongee kwa ajili ya wananchi wa Ikungi, Ikungi maji salama ni asilimia 25 tu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Wizara hii leo niwasemee akinamama, naomba maji yaende Ikungi hawana mtetezi humu ndani, kwa sababu mtoto wao kahamia kwa Wazungu. Kwa hiyo, naomba sana maji yaende Ikungi. Hakuna barabara kule, umeme ambao umepelekwa kule ni vijiji 44 tu kati ya… (Makofi/Kicheko)

MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana na mimi kwa kweli naomba nijielekeze kuwatetea wanawake wa Mkoa wa Singida hususani wa Jimbo la Ikungi Mashariki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali ya Makyungu iko Singida Mashariki. Hospitali ya Makyungu mpaka sasa hivi huduma za maji pale ni hafifu, naomba sana Wizara kwa sababu Hospitali ile imekuwa ikitoa huduma nzuri sana na kuna ongezeko la watu, naomba Wizara iiangalie kwa jicho la pekee kupeleka maji pale Makyungu ili yaweze kuhudumia wananchi wanaoishi maeneo yale. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimezungumza haya bado nitashukuru sana kwenye Jimbo la Singida Magharibi pale Sepuka, kuna mradi wa maji mkubwa ambao umepelekwa pale, kwa hiyo naishukuru sana Wizara kwa sababu wamepeleka milioni 101, naamini zitasaidia maeneo yale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeyasema haya kwa sababu nafahamu kazi kubwa ambayo anaifanya Rais wetu, anapaswa kuungwa mkono na watu wanaowatetea wanyonge. Kama kweli wewe ni mtetezi wa wanyonge utapaswa umuunge mkono Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli. Nasema haya kwa sababu mpaka sasa hivi tunavyoongea akinamama wa Singida hususani Singida Mashariki wanashindwa kwenda kujifungulia kwenye Vituo vya Afya kwa sababu huduma kule hazipo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii Rais wetu ameamua kulinda rasilimali za Taifa letu ili ziende zikaokoe hata wale akinamama wanaofia njiani kwa sababu ya kushindwa kwenda kwenye vituo vya afya, mtu anasimama anasema amekosea, inauma sana! Nampongeza Rais wangu na tutaendelea kumuombea na nataka kusema hivi, nawapongeza wale wanaompongeza, hata neno la Mungu linasema ni heri uwe baridi au moto kuliko kuwa vuguvugu, kwa sababu ukiwa vuguvugu kinywa cha Bwana kitakutapika, unaelewa maana ninayoisema hii. Ni lazima tumuunge mkono Rais wetu katika juhudi hizi anazozifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mkoa wetu wa Singida, bomba la mafuta linaloenda Tanga, linapita katika Wilaya tatu katika Mkoa wetu wa Singida, wananchi wa Singida wanakwenda kunufaika na juhudi kubwa ambazo zimefanywa na Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais wetu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme hivi, mwizi ni mwizi tu, iwe umeweka mkataba mbovu, usiwe mbovu, mwizi ni mwizi na akikamatwa achukuliwe hatua. Nilimsikiliza Rais wetu, ameonesha huruma kubwa sana amesema jamani njooni tuzungumze ili mtulipe pale mlipoona mmetuibia tatizo liko wapi? Naomba tumpongeze Rais wetu ili hawa watu ambao naamini kesho na kesho kutwa tutawaona wanaenda kutaka suluhu kwa ajili ya kutulipa, kwa hiyo nataka nimpongeze Mheshimiwa Rais wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine pale Londoni na pale Sambaru huko Mashariki ya Singida, kuna matatizo makubwa ya wachimbaji wadogo, nategemea tusimame kuweza kuwatetea wachimbaji wadogo pale, tukimuunga mkono Rais wetu, hata wachimbaji wetu wadogo pale watanufaika na mradi uliopo pale. Mwekezaji aliyepo pale tangu 2006 mpaka sasa hajalipa compensation, mpaka sasa wananchi wanahangaika, naomba sana tumuunge mkono Rais wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni kengele ya kwanza, kabla sijamalizia nataka nimalizie kwa kusema hivi, Mheshimiwa Magufuli songo mbele, ukiona watu wanakupinga, ujue kuna jambo limejificha nyuma yao, ama wanaona aibu na upinzani wa kupinga kila kitu utajipinga hata wewe mwenyewe, kuna mambo ambayo utayasema leo kwa sababu ya kupinga, utapinga kesho. Mheshimiwa Rais wetu naomba usonge mbele, wanaokupinga ni kwa sababu wanaona nchi hii inakwenda kupaa, nchi hii inakwenda kunufaika na kwa sababu wanapinga na ni wachache wala hawatuwezi humu ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimalizie kwa kusema hivi, ngoja nikae sawa…..

(Hapa Mheshimiwa Mbunge aliimba -Kanyanga twende Magufuli wetu, Kanyaga twende, usiogopeeee)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.