Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kuchangia bajeti hii. Kwanza nianze kwa maneno yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Watanzania wanapoenda kuchagua viongozi na wanapoenda kupiga kura ya kumchagua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wanamchagua mtu ambaye wanamkabidhi dhamana juu ya usalama wao, uhai wao, usimamizi wa rasilimali zao. Huyu anakuwa custodian wa resources zao ambazo wamekuwa nazo walizopewa na Mwenyezi Mungu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais ameunda Tume mbili na ametusomea findings za Tume zake, lakini huko nyuma Marais nao waliunda Tume mbalimbali. Nataka nitumie Bunge hili kuwaambia Waheshimiwa Wabunge wenzangu, vita ya kupambania rasilimali ya nchi hii siyo vita ya John Pombe Magufuli, vita hii ni vita ya Watanzania wote. Naamini kwamba there is no wrong doing in doing right thing, hakuna kufanya makosa katika kufanya jambo jema. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jana baada ya kuchangia kaka yangu Mheshimiwa Tundu Lissu mimi nilimfuata kwa heshima kabisa ili anipatie maandiko yake. Mpaka saa tisa usiku jana nimekuwa nasoma baadhi ya maandiko yake. Ukisoma ripoti ya Bomani, ukisoma writing alizoandika kaka yangu Mheshimiwa Tundu Lissu na mkononi hapa ninayo kesi ambayo yeye aliisimamia ya mwaka 2006, this country imeibiwa rasilimali zake kwa muda mrefu. Nataka niombe Bunge hili, let’s not be hostage of the history. Bunge hili limefanya makosa, viongozi wetu huko nyuma wamefanya makosa, leo tumepata mtu anayetu-lead kwenda kupambania haki zetu let us join hands with him. Tumnyooshee mkono akishindwa kutufikisha mwisho wa vita hii, not now! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi natoka Nzega, katika kesi hii kaka yangu Mheshimiwa Tundu Lissu anawafahamu akina Mzee Jumbe Kumega, anamfahamu Mama Fatuma Mhina wa Isungangwanda amewa-cite, these are victims. Leo kama Mbunge wa Jimbo la Nzega Mjini ndugu yangu Mheshimiwa Kigwangalla alipigwa mabomu kwa ajili ya Resolute.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeibiwa na kama alivyosema Mheshimiwa Heche jana na mimi nataka niseme leo, Resolute ameondoka na fedha za Halmashauri ya Nzega ten billion shillings za service levy. Jambo la kusikitisha Serikali imeipa kampuni tanzu ya resolute leseni ya kupewa maeneo ndani ya Jimbo la Nzega, Wallah wabillah watallah, kama hamtafuta leseni ya Mwabangu Miners, mimi nitaongoza wananchi I will not care the outcome! (Makofi)

Mheshimiwa Menyekiti, pili, namwomba Mheshimiwa Mpango, yeye ni Waziri wa Fedha, Resolute wana mgogoro na TRA juu ya kodi! Kuna ten billion yetu kaka yangu Mheshimiwa Dkt. Kalemani anaijua. Nataka kwenye wind up waniambie ten billion ya Halmashauri ya Nzega inapatikanaje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Rais amesema nasi lazima tumuunge mkono na katika hili la Resolute nitamuunga mkono kwa jitihada zangu zote. Asiponijibu Mheshimiwa Kalemani, kile chuo walichofungua cha madini naenda kuwaambia wananchi wagawane yale mabati, that is all we can get wananchi wa Nzega. Tumeachiwa mahandaki yenye urefu wa zaidi ya mita 1,000, tunaambiwa yatajaa maji baada ya miaka 200 we will not allow this.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme Rais amekuwa mstaarabu sana, angetangaza kufunga hii migodi, leo kuna Diamond Williamson, walichokifanya Diamond Williamson pembeni kuna uchimbaji unaendelea wa kampuni nyingine ya Hilal, yule Hilal kapewa kazi ya ulinzi wa migodi ya Diamond, wanachukua almasi kutoka kwenye mgodi wa Mwadui wanaenda ku-process kwenye mgodi wa Hilal zinaondoka kwa njia za panya, this has been the game for years, this business has to stop! Lazima tumuunge mkono Rais katika hili, tuje tumnyooshee mkono akishindwa kutufikisha mwisho. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nijielekeze kwenye hoja ya kaka yangu Mheshimiwa Dkt. Mpango, sina mgogoro mkubwa na yeye this time, namuunga mkono nina mambo machache ya kushauri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nishauri kwenye hotuba ya Mheshimiwa Dkt. Mpango; kwenye page namba 50 ametaja sheria anazokuja kutuletea kwa ajili ya kuzifanyia mabadiliko. Sheria ya kwanza ni Sheria ya Kodi ya Ongezeko la Thamani Sura ya 148. Hapa tunaona dhamira ya Serikali ya ku-link industrialization na fiscal measures za nchi. Serikali inafuta VAT on capital goods ni jambo zuri, namwomba Mheshimiwa Waziri a-extend hii iwe ni capital goods with processing chemicals, kwa sababu chemicals ambazo tutakuwa tuna-import kwa ajili ya ku-process kwenye viwanda bado zitakuwa na import duty tax.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tunapofuta kodi ya ongezeko la thamani kwenye capital equipment tufute na kodi zinazoendana na chemical goods ambazo zitatumika katika viwanda vifuatavyo: Viwanda vinavyohusika na mazao ya kilimo hasa ya nguo, kwa maana ya viwanda vya cotton vinavyo-process nguo ili tu-link na mpango wa Serikali wa cotton to clothes (C to C) ambao umeandikwa na Serikali. Hilo ni jambo la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, tufute kodi ya import duty kwenye chemicals zinazotumika ku-process leather industry. Nchi yetu ni ya pili kwa mifugo, itakuwa it is not helping kama hatutaweza ku-take hii advantage, kwa sababu asilimia 65 ya watu wetu wako kwenye sekta ya kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kodi ya pili ambayo nataka nishauri ni kodi ya mapato. Tumepunguza kutoka asilimia 30 kwenda asilimia 10 ya corporate tax, lakini maeneo gani? Ni assemblies ya matrekta na magari. Namwomba Mheshimiwa Waziri, tu-extend hii docket, tutatoa hii fiscal incentive ya asilimia 10 ya corporate tax kwenye viwanda vyote ambavyo vitawekeza kwenye korosho, vitawekeza kenye mazao ya kilimo kwa maana ya kwamba cotton, korosho, kahawa kwa sababu leo korosho yetu yote inakuwa exported raw kwenda India. Hii haitusaidii, maana yake ajira zinakwenda nje. Kwa hiyo, naomba docket hii iongezwe zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Mheshimiwa Waziri kwenye VAT, leo mkulima wa alizeti akizalisha alizeti, akisindika tu anakutana na VAT. Ningemwomba Mheshimiwa Waziri, ili tuweze ku-gain advantage ya kukua kwa viwanda, iweze kuchukua watu wengi, mazao ya kilimo yanayosindikwa ndani tufute kodi ya VAT katika mazao haya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria ya Fedha ya Serikali za Mitaa, Sura ya 20, wenzangu wameongelea sana suala la CESS. Mheshimiwa Waziri nataka niwaombe kuna kodi inaitwa services levy ya asilimia 0.03 ya gross income. Kodi hii inakwenda kinyume na principle of taxations, kwa sababu tunachaji kodi kwenye mtaji, sheria hii ilifanyiwa mabadiliko mwaka 2012 Sura ya 6, tukasema kila Mtanzania mwenye leseni pato lake la mwaka (Gross income) linachajiwa asilimia 0.03, kwanza ina-attract double taxation kwa sababu service levy hii inachajiwa kule juu lakini kwa mzalishaji, vilevile na muuzaji wa Nzega anachajiwa. Tufanye nini? Tuweke dermacation, tutengeneze levels, kwamba service levy ichajiwe 0.01 kwa wafanyabiashara wadogo wenye leseni, corporate wabaki wachajiwe 0.03. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria ya Forodha ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. Sheria hii tumei-impose asilimia 10 kwenye crude oil. Najua kuna a lot of politics kwenye suala la mafuta ghafi, lakini ukisoma ripoti ya BOT ya mwezi Aprili re-exportation imeshuka. Nchi za jirani wenzetu wamefuta! Matokeo yake sisi tunakuwa soko la mafuta kutoka Kenya na maeneo mengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Mheshimiwa Waziri, udhaifu wa taasisi zetu za kusimamia shughuli wanazowapa usiathiri uzalishaji, kwa sababu sasa hivi ni kwamba kuna udhaifu inawekwa kodi ili ku-discourage kama walivyofanya kwenye sukari za viwanda. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuomba dakika moja kama muda wangu umekwisha. Naomba niongelee kodi ya railway development…

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mbunge, muone baadaye Waziri tunakwenda kikanuni.

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.