Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Bhagwanji Maganlal Meisuria

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. BHAGWANJI MAGANLAL MEISURIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, Mungu akuweke. Nimepata nafasi hii kuzungumzia bajeti yetu ya Serikali. Nataka niseme sisi Wabunge wote hakuna ubaguzi wa rangi wala Kabila tunaunga mkono bajeti ya Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawapongeza Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu wake. Hicho kitabu alichoandika cha bajeti ya Wizara ya Fedha na Mipango, namuunga mkono, Mungu amweke. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana sana Mheshimiwa Rais wetu Dokta John Pombe Magufuli, amefanya kazi nzuri, kwa sababu tulikuwa tunadhulumiwa madini yetu yanakwenda nje. Mungu ameweka neema yake awamu yake akafanya vizuri na anasaidia kuondoa umaskini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais wetu Magufuli amefanya mambo mengi, ujenzi wa barabara, uwanja wa ndege na ameleta ndege mbili na analeta ndege nyingine nne. Hayo yote yatasaidia kuondoa umaskini kwa sababu itaongeza mapato. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, akinamama wa Zanzibar pamoja na Watanzania wote wamechoka kubeba mizigo ya maji, pesa hizo zitasaidia wananchi wetu wa Tanzania tutoke kwenye umaskini twende katika hali nzuri. Inshallah, Mwenyezi Mungu atampa nguvu Rais wetu Mheshimiwa Magufuli na ataondoa shida zetu zote na maji yatapatikana kwa kila mmoja wetu, Zanzibar pamoja na Bara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nazungumzia Halmashauri, Halmashauri zetu wanakusanya pesa, tuwasimamie vizuri lakini naomba Serikali zile pesa milioni 50 tuzipeleke kwenye Halmashauri. Wananchi wanangoja kwa hamu pesa zile kwani zitasaidia kuondosha umaskini na tutasaidia wale watu waliokuwa na shida kwenye ushirika, asilimia nne au tano walikuwa wanapata na kukopeshwa basi Serikali isaidie. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali pamoja na Rais wetu amefanya kazi nzuri kwa kuanzisha mabasi ya mwendokasi, Watanzania wamekuwa wakifaidika. Pia tunaingiza pesa chungu nzima na pesa hizo tutaziweka katika kilimo, maji pamoja na mambo mengine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni viwanda, kweli nasema Serikali inajitahidi kusimamia viwanda. Kwa kuwa na viwanda itasaidia sana wananchi na vijana wetu kupata ajira na ajira ni muhimu kwa Tanzania yetu. Kwa kuanzisha viwanda mbalimbali mapato ya Taifa yataongezeka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, TRA yetu lazima isimamie ukusanyaji wa mapato. Mapato yapo kwenye viwanda, sekta ya utalii na bandari, haya yote tuyasimamie. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine naomba Serikali yangu ya Muungano tuwasaidie watu wa Zanzibar. Mwenzangu Mheshimiwa Rehani amesema lakini mimi nazidi kusema sisi wote ni ndugu moja, hakuna upinzani wala ubaguzi. Wale watu wanyonge kutoka Zanzibar wanaleta biashara ndogo ndogo, wanatoa ushuru kule lakini ikifika hapa wanahangaishwa, basi tuwatazame na tuwaachie.

Wazanzibar tuwaache wafaidike kwa sababu kule Zanzibar unalipa ushuru namna mbili, ZRB pamoja na TRA. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Mheshimiwa Waziri tuboreshe biashara za viwanda. Kama tutasimamia kweli Tanzania yetu tutapata mapato mengi sana, asidharau. Vilevile tunataka tufufue viwanda vyetu, wale watu wanakuja kutoka nchi za nje wanataka kuanzisha viwanda tuwapokee. Hii ni kwa sababu vijana wetu watapata ajira na kuondokana na umaskini. Vijana wakifanya kazi na nyumbani akipeleka chochote itasaidia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kusema kitu kimoja, sisi Zanzibar pamoja na Tanzania yetu tuna mambo mengi sana ya kusaidia kuingiza pesa. Tanzania tunazalisha mazao kama kunde, choroko na dengu, tunao watu kutoka nchi za nje kama India wanakuja kununua tuwakaribishe. Sisi tunataka maendeleo na mapato. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mheshimiwa Waziri ameondoa kodi katika mazao ya kilimo kwa tani moja. Vilevile ameondoa kodi kwenye magari, tunamshukuru sana Mungu amweke. Serikali yetu inataka kufanya mambo, tumuunge mkono Rais wetu Mheshimiwa Dokta John Pombe Magufuli kwa sababu Mheshimiwa Waziri… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji