Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa. Awali ya yote nianze kwanza kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa namna ambavyo amekuwa akifanya shughuli zake ndani ya Bunge na nje ya Bunge na niwapongeze Mawaziri wanaomsaidia katika ofisi yake, Mheshimiwa Jenista Mhagama na niseme tu Mheshimiwa Jenista lile tatizo la maji Nzega kule mpaka leo mambo muswano. Kwa hiyo, nakushukuru sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nimshukuru sana Mheshimiwa Antony Mavunde kwa kazi anazofanya na commitment anayoonesha na namna ambavyo amekuwa akijituma katika kufanya shuguli zake. (Makofi)

Mheshimiwa Mweiti, nianze kwa maneno yafuatayo. Ukitazama ngao yetu iliyoko mbele yetu pale ina maneno mawili, uhuru na umoja. Mwaka 1957 wazee wetu wakiwa pamoja na kijana wao wakati huo Mwalimu Julius Kambarage Nyerere walipoanza harakati za kutafuta uhuru kupitia Chama cha TANU waliwaunganisha Watanzania wote kwa makabila yao, dini zao ili kupata umoja ambao utafikia dhamira ya wao kupata uhuru wa Tanganyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, yapo mambo ambayo yanaendelea katika nchi yetu ambayo yanaashiria kuanza kuwepo kwa migawanyiko katika Taifa letu. Mambo haya tukiendelea kuyatazama kwa macho hayaleti taswira njema huko mbele na wala hayataweza kulifanya Taifa hili kuendelea kuwa Taifa moja na kupambana na adui mkubwa ambaye ni umaskini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, yanatokea matukio ya kusikitisha katika nchi yetu ambayo ukitazama huoni any concern ya deliberate effort ambayo itawajengea Watanzania imani kwamba, hata mimi mdogo nikikumbwa na zahma basi yupo anayenilinda. Yamekuwa yakitokea matukio mengi yakikosa majibu katika nchi yetu, lipo tukio la kijana anaitwa Allan ambaye ni muuza machungwa pale Mbeya. Mimi ningeiomba Serikali kwa heshima kabisa, matukio ya namna hii yakiendelea kujengeka katika nchi yetu na ku-develop culture ya impunity yana-destort peace iliyopo katika Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kijana huyu amekufa. Ripoti ya Daktari Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Mbeya imesema kwamba kijana huyu kafariki kwa majeraha ya ndani ya mwili wake. Familia yake imesema waliomuua, waliompiga ni Jeshi la Polisi. RPC wa Mbeya akasema hawahusiki! Matokeo yake nini, Serikali imeenda kutoa rambirambi ya shilingi 200,000. Is that the reason? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, matukio ya namna hii yameendelea kuwepo, mimi ningeiomba Wizara ya Mambo ya Ndani na Ofisi ya Waziri Mkuu, Serikali wakati ina-wind up budget ya Waziri Mkuu waagize kuundwa kwa official independent organ ifanye investigation ya haya mambo. Hatuwezi kuacha this culture of impunity inaendelea katika nchi yetu, it is very sad na ina-destort image. Hii ndiyo inatumika na watu wasiopenda nchi yetu kuendelea kuharibu heshima ya Taifa letu. Hili ni jambo ambalo ninaiomba Serikali ichukue hatua katika jambo hili. Kwa hiyo, hili ni jambo la msingi sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nirejee kwenye hotuba ya Waziri Mkuu, Waziri Mkuu katika hotuba yake ameelezea kukua kwa uchumi. Rais anafanya effort nyingi ku-encourage watu kujenga viwanda katika nchi yetu, kama hatutaamua deliberate kuwa na specialisation hatuwezi ku-specialise katika kila jambo, 70% ya nchi yetu iko katika sekta ya kilimo. Nitoe mfano, mwaka 2015/2016 uzalishaji wa zao la korosho na Serikali imesema kilimo kimekua kwa asilimia 3.6. Uzalishaji wa korosho ulikuwa tani 265,000 msimu huu tunazungumzia tani 313,000 inputs ambazo Serikali iliingiza, investiment ya Serikali ni shilingi bilioni 28 kwenye zao la korosho. Msimu uliopita mapato tuliyoyapata ni bilioni 872. Serikali ilivyoamua ku-invest 28 billion mapato ya korosho sasa hivi yatakwenda
1.18 trillion shillings. Waziri wa Fedha haoni hili? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, it is not a rocket science, narudia. Kilimo tulizungumzia NFRA, Wizara imeomba 86 billion shillings, inapewa 15 billion shillings. Mwaka huu tunazalisha metric tones 900,000 mahitaji yetu ni metric tones
5.9 hii excess inaenda wapi? Tutafunga mipaka ili tu-create artificial control ya inflation tuseme mfumuko wa bei asilimia nne, tunawatia umaskini wakulima. We have to be serious. Inputs kwa ajili ya pamba Wizara imeomba 10 billion Serikali imempa three billion. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo wale wadudu wanaokula mahindi wanaitwa viwavijeshi wameshaanza kushambulia baadhi ya maeneo. Kwa nini, kwa sababu, fedha zilizoombwa na Wizara ya Kilimo kwa ajili ya inputs hawajapata as per the requirements. What do we want? Tunataka nini? Siyo muujiza, tukijenga viwanda kama asilimia 70 ya Watanzania ni maskini, hawana uwezo wa kununua bidhaa za viwanda hivyo, viwanda hivi vitakufa tu na wala siyo muujiza. Nataka niiombe Serikali, nimesoma mpango wa Dkt. Mpango, nitakuja kuongea wakati wa bajeti, it is typical cosmetic measures. Hakuna serious fiscal measure zinazotengenezwa na Wizara ya Fedha kuweza ku-stimulate sekta ya kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tunaagiza crude oil karibu tani 600,000. Nini mpango wetu wa kuwekea kwenye mazao ya alizeti, ili tuweze kujitosheleza mafuta? Kama hatutaamua, nitoe mfano wa mifugo. Kwenye hotuba ya Waziri Mkuu amezungumzia suala la chapa na mimi nimpongeze Ndugu yangu Mheshimiwa Ulega kwa mara ya kwanza kajua, zamani ng’ombe alikuwa anaita mnyama siku hizi anaita mifugo, kawajua na ng’ombe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili tuweze ku-improve mazao yanayotokana na mifugo ni lazima tuwekeze kwenye proper breeding programs. Ng’ombe wetu hawajafanyiwa breeding toka mwaka 1982, hakuna investments, leo mzalishaji wa maziwa anayezalisha maziwa, mfano mtu kama ASAS, cost of production ya ASAS ni asilimia 18 juu kuliko mzalishaji anayezalisha maziwa Kenya. Kwa nini? Ni kwa sababu ya mfumo wetu wa kodi. Nataka nijiulize Serikalini kwa nini mnahitaji VAT kwenye vifungashio vya maziwa? Why?

Mheshimiwa Mwenyekiti, zimeisha dakika? Naunga mkono hoja.