Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Stephen Hillary Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kuunga mkono hoja

iliyoletwa hapa mezani na aliyoyaongea yote Mheshimiwa Waziri Mkuu nimpongeze sana kwa kazi nzuri wanayoifanya Serikali hii ya Awamu ya Tano. Vile vile nimpongeze sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwamba kumbe inawezekana. Amefanya mambo makubwa na yameanza kuonekana ndani ya Tanzania na nje ya Tanzania. Mungu ambariki sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa suala la reli. Reli ni kichochea kikubwa sana cha uchumi Tanzania, lakini niombe, sitashika shilingi tena kama mwaka jana; mwaka jana nilishika shilingi kwa ajili ya reli ya kutoka Tanga-Arusha
– Musoma ila nataka Waziri husika katika suala la reli ahakikishe safari hii hakuna haja ya kushikiana shilingi atuambie; tunahitaji standard gauge lakini huwezi kujenga zote kwa wakati mmoja, lakini ni namna gani reli ya kutoka Tanga kupitia Kilimanjaro, Arusha na kwenda Musoma itaanza kazi ili na sisi mizigo yote ambayo ilikuwa inatoka katika bandari ya Tanga ifanye kazi nzuri? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nirudi kwenye Bomba la Mafuta, tumshukuru sana Rais. Bomba la Mafuta lingeweza kwenda mkoa wowote lakini limeletwa Tanga kutoka Uganda. Naomba sana Serikali hii sikivu wajaribu sana Watanzania wapate kazi pale, ule mtaji wa kwamba Watanzania wanalishangilia bomba la mafuta wanaokuja kufanya kazi ni Wakenya uwe sasa mwisho. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna kawaida ya watu wanatengeneza biashara kama hizi vijana wa Kitanzania hasa wa Mkoa wa Tanga na jirani na wanakopita Bomba la Mafuta hata kuchekecha zege watolewe watu Kenya, hata kushika lile toroli mtu atoke Kenya! Safari hii haiwezekani, wakija kwetu watu wa namna hiyo tutawafukuza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwombe Mheshimiwa Waziri Mkuu msikivu sana, kuna Watanzania waliamua kujenga shule za kata; shule za kata zimejengwa maabara nyingi na Watanzania wenyewe kwa nguvu zao wenyewe. Naiomba sana Serikali, kwa sababu tunataka watoto wetu
wasome tuangalie ni mazingira gani watatengewa fedha, zile sehemu zote ambazo wananchi walitumia nguvu kubwa sana kujenga maabara za kata katika shule za sekondari watenge fedha ambazo watamalizia nguvu za wananchi wenyewe walioamua kujitolea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili nimeona niliseme kwa sababu wananchi waliamua wenyewe kujenga shule za kata lakini mpaka leo hii kuna magofu ya ajabu sana katika shule za kata, hakuna mahali ambapo utaenda utakuta maabara, na vijana wengi lazima waingie kwenye maabara kujifunza sayansi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la REA ni suala la msingi sana katika Tanzania. Tunategemea sana kwamba umeme utakwenda vijijini, lakini cha kusikitisha utashangaa kuona REA tulipewa taarifa kwamba katika kila wilaya kutakuwa na vijiji ambavyo vitapata REA na tukashukuru sana. Hata hivyo, hatua ya mwisho unakuja kuambiwa vijiji vile vimekatwa, wananchi wanaanza kulalamika kwamba Waheshimiwa Wabunge hatuwatendei haki, kwa nini vijiji fulani vimekatwa na ni kwa nini mlituambia kwamba vijiji hivi vitapata REA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia kwenye simu yangu hapa, ukinunua bando unaambiwa umekatwa shilingi fulani za kwenda kwenye REA. Ukiwauliza watu wanaosimama kujenga au waliopata contract za kusambaza umeme wanakwambia hatujalipwa. Sasa najiuliza hii hela inayokatwa kwenye simu hii ambayo inaonesha kabisa inaenda kwenye REA, sasa inakwenda wapi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri husika, Mheshimiwa Waziri Mkuu vijana wake wamekuja Jimboni kwangu Mawaziri zaidi ya kumi (10) na nawashukuru sana wamenifanyia kazi nzuri sana. Wamekuja wametoa fedha nyingi sana; na kwa sababu katika Tanzania Korogwe ni wilaya ya kuigwa kwa sababu tukipewa hela chache tunafanya kazi kubwa na chenchi inabaki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba mziangalie zile wilaya ambazo zina uchungu na fedha ya Serikali kwa macho yote ili mtusaidie kutengeneza zile sehemu ambazo zimeanza. Leo tunajenga kule vituo vya afya, kuna vituo vya afya vizuri na kuna shule za sekondari nzuri ambazo hata Waziri wa Elimu, Waziri wa Nishati, Waziri wa Ardhi, Waziri wa Kilimo, Waziri wa Maji, Mawaziri karibu wote wamekuja pale na wameona. Naomba sasa ...

T A A R I F A . . .

MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Tena nimeipokea kwa mikono miwili ahsante sana ndugu yangu.

MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Naipokea, tena kati ya watu ambao wamenisaidia sana Wizara ya Nishati ni huyo Naibu Waziri.

Alifika akafanya kazi nzuri sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunakwenda kwenye upande wa Maji. Taarifa zote nimezipokea, ya huyu niliipokea kwa vizuri na Mheshimiwa Waziri kwa sababu amefika mpaka jimboni kwangu na amelizungukia jimbo lote na ameona haya matatizo, zote nazipokea na ninaomba Serikali izifanyie kazi. (Makofi)

T A A R I F A . . .

MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana unilindie muda wangu, umeona wengine hapa, haya. (kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye suala la REA nafikiri wenzangu wamenisaidia na Waziri amenisaidia, tuje kwenye upande wa TARURA. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili TARURA ni kama jipu, tulilipendekeza sisi hapa kwamba TARURA itufanyie kazi sasa ipewe kazi ya kutengeneza barabara lakini mpaka leo hii kwangu hawajatengeneza barabara hata moja. Kuna daraja limekatika kutoka Kwa Sunga kwenda Mswaha darajani, miezi tisa daraja halijajengwa hata kujengwa tunaambiwa kuna TARURA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mji wa Korogwe unategemea sana Mji wa Mombo kupata fedha ya kuendesha Wilaya ya Korogwe, lakini leo hii mtu aende mpaka Mombo akaangalie barabara zilivyo leo tunaambiwa kuna TARURA, hawa TARURA ni mtu binafsi? Kama ni chombo ambacho kimeundwa kwa ajili ya kusaidia Serikali ina tatizo gani kwenda kutengeneza barabara ambazo zimekufa? Ni nini kinazuia wakati kuna fedha tayari wameshatengewa na Serikali? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii TARURA naomba ieleweke kabisa kwamba TARURA pamoja na kwamba wanadai kwamba wametengewa fedha hizo fedha ziko wapi? Kama zipo kwa nini hawatengenezi barabara za vijijini? Tumeziondoa kwenye Halmashauri kwa sababu walikuwa wanataka sana ten percent, tukawapa TARURA ambao hawaingiliwi na mtu yeyote. Sasa kama hawaingiliwi na mtu yeyote, fedha zikae mifukoni mwao?

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee suala la maji, suala hili ni kigezo kikubwa sana kwa sisi Watanzania, Mbunge yeyote atakayefika jimboni kwanza unaulizwa maji. Kuna maji toka mwaka 2010 ambayo yanatoka Mkoa wa Kilimanjaro, Bwawa la Nyumba ya Mungu, hili mpaka leo hatujui yameishia wapi. Tunasikia tu mradi unaendelea, mradi unaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna miradi ya Benki ya Dunia, tangu mwaka 2010 mimi naingia Bungeni mpaka leo imesimama. Leo tunasema maji vijijini haya maji vijijini wanapata kina nani? Naomba sana Serikali ile miradi yote ambayo imeanzishwa na baadhi ya viongozi wamepita na kui-support naomba ikamaliziwe kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapata shida sisi Wabunge, unafika mahali unawaambia maji yanakuja, unakwenda siku ya pili wanakwambia maji yako wapi? Unafika mahali unawaambia barabara ya lami kutoka Korogwe kwenda Lushoto kupitia Bumbuli itatengenezwa, mwaka wa 10 huu mtu anakuangalia anakwambia barabara ichongwe. Unafika barabara za vijijini zimekufa; unafika suala la vituo vya afya; tunawashukuru sana Serikali hii imetenga fedha taslimu kwenda kwenye madawa kwenda kwenye vituo vya afya, lakini kuna vituo vya afya vingine vimeshaanza kuleta nguvu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, Hospitali ya Magunga ya Korogwe, ndiyo hospitali kubwa katika barabara kuu hii, haina gari. Magari yalikuwepo yamekufa na ndiko kwenye ajali kubwa zinazopatikana barabara ya kutoka Chalinze kwenda Kilimanjaro, wanapitia pale, hakuna gari. Naomba Serikali iiangalie Korogwe kwa macho ya ukunjufu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuja kwenye suala la katani. Katika mazao makuu ya biashara katika Tanzania yamewekwa manne, naomba liwekwe na katani. Katani ni zao kubwa ambalo limeingiza fedha, sisi wengine Tanga tumekwenda mwaka 1961 tukiwa manamba tumefuata Katani. Katani ilikuwa inaingiza fedha kuliko zao lingine lolote, lakini cha kushangaza mpaka sasa hivi katani hii wanaoendeleza ni watu wachache wakulima binafsi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wenzetu hawa ambao wanajiita Bodi ya Mkonge wameyajaza mashamba. Katika Tanzania eneo lenye mashamba makubwa ya Mkonge ni Korogwe Vijijini, nina mashamba zaidi ya 18; watu hawaendelezi, wanaoendeleza ni watu walioshika mashamba binafsi akina Mohamed Mo, Mura, Luhinda pamoja na Gai; lakini ukiangalia mashamba ambayo yameshikwa na hawa wenzetu wa Bodi ya Mkonge hakuna shamba hata moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi si kwamba tunakataa katani, tunaipenda sana katani hata juzi Waziri wa Kilimo amefika pale na kuwakemea sana, lakini yale mashamba ambayo hayaendelezwi wapewe wananchi walime Mkonge. Tunakuwa tukisema mkonge, mkonge, mkonge wenyewe kwa mkulima mdogo kwenye katani ananunua kwa shilingi elfu nne wakati watu…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)