Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi niweze kuchangia katika hotuba hii ya Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia uzima, lakini pia nichukue nafasi hii kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na naomba nichukue dakika moja kumuombea katika kazi anazozifanya naanza kwa kusema Baba katika jina la Yesu, damu ya Yesu imfunike Dkt. John Pombe Magufuli, imfunike Majaliwa, imfunike Jenista Mhagama, ifunike Mawaziri wote, ifunike Serikali ya Tanzania ninakushukuru Baba wa Mbinguni kwa sababu Serikali ya Tanzania inafanya kazi kwa jinsi watu wanavyoitaka wote tuseme Amen.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze sasa kwa kuchangia katika Wizara ya Elimu. Mkoa wa Rukwa hauna Chuo cha VETA. Chuo cha VETA kimezungumziwa muda mrefu sana lakini mpaka sasa hivi hakuna kinachoendelea nataka kujua tatizo ni nini? Mheshimiwa Waziri atakapokuja kuleta majibu hapa atuambie kuna tatizo gani kuanzisha chuo cha VETA katika Mkoa wa Rukwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee maabara, Serikali ya John Pombe Magufuli ilianzisha kujenga maabara katika shule za sekondari na ilikuwa na nia nzuir lakini mpaka sasa hivi maabara nyingi hazijaisha tatizo ni nini watoto wanaotaka kusoma chemistry, science wanashindwa kupata elimu nzuri, ninaomba Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi safari hii kwenye bajeti hii iweke fungu la maabara ziishe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee suala la walimu, tangu zoezi hili la kuwabadilisha walimu wa sekondari waende wakafundishe kwenye shule za msingi limeleta shida kidogo kwa sababu shule za sekondari sasa zimepungukiwa na walimu. Nilikuwa naomba Serikali ifanye haraka kuwaajiri walimu ili shule za sekondari sasa ziweze kukidhi mahitaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee suala la ukubwa wa Mkoa wa Rukwa, Mkoa wa Rukwa una majimbo matano, lakini kuna majimbo mawili ni makubwa sana nataka niongelee Jimbo la Kwela, jimbo la Mheshimiwa Malocha, jimbo lile lina kata 27 limejigawa Ufipa wa Juu na Ufipa wa Chini. Ufipa wa Juu una kata 14 na Ufipa wa Chini una kata 13. Mheshimiwa Malocha amekuwa akifanya kazi ngumu sana na kubwa, lile jimbo ni kubwa sana na ameliongelea muda mrefu kwamba tunaomba basi ligawanywe kwa sababu wananchi wanashindwa kupata huduma kwa wakati. (Makofi)

Mheshimiwa Mweyekiti, ukianza Ufipa wa Chini ukizungukia Ufipa wa Chini kabla haujamaliza unapandisha Ufipa wa Juu unakuwa umeishiwa mpaka mafuta. Ufipa wa Juu wanaanza kulalamika kwamba Mbunge hatufikii sisi hapa watu wa Ufipa wa Juu ni kwa sababu lile jimbo limekuwa kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni sawa na jimbo la Mheshimiwa Kandege na lenyewe lina kata 27 nilikuwa naomba kwa sababu hili linatuletea shida sana hata kwenye upande wa kisiasa.